Kufuatia kufanya vizuri msimu huu katika michuano ya Klabu Bingwa Africa, klabu ya Simba imeipatia Tanzania nafasi nne za kushiriki michuano ya vilabu inayoandaliwa na Shirikisho la Soka barani Afrika msimu wa mwaka 2020.
Simba imefikia hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kabla ya kuondolewa na TP Mazembe, ambapo imefikisha jumla ya pointi 18 na kuisaidia Tanzania kupanda hadi nafasi ya 12 ya ubora wa vilabu barani Afrika. Pointi tatu kati ya hizo 18 zikitokana na Yanga kufuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho katika mwaka 2016 na 2018.
Gor Mahia ya Kenya ambayo ilikuwa ikishiriki michuano ya Shirikisho barani Afrika, imeondolewa na klabu ya RSB Berkane ya Morocco na hivyo kushindwa kuongeza pointi zaidi baada ya kuwa na pointi 14 kwenye hatua hiyo iliyoishia.
Kwanini Tanzania inapeleka timu nne 2020 na sio 2019?
Kanuni zinasema kuwa nchi itakayofikia pointi 12 katika msimu wa michuano ya vilabu barani Afrika, baada ya misismu miwili itapata nafasi ya kuingiza klabu nne katika michuano hiyo inayoandaliwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika, CAF.
Endapo Gor Mahia ingeshinda mechi yake ya robo fainali na kufuzu hatua ya nusu fainali, ingeipokonya Tanzania nafasi ya kupeleka timu nne katika michuano hiyo. Kwa maana hiyo sasa, Tanzania itapeleka timu mbili katika Klabu Bingwa Afrika na timu mbili katika Kombe la Shirikisho katika msimu wa 2020/2021.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...