Wednesday, April 10, 2019
CAG azibana CHADEMA, CCM kwenye ripoti
Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali, Prof. Mussa Assad, katika ukaguzi uliofanyika katika vyama vya siasa, CCM ilibainika kuwa haijawasilisha makato ya wafanyakazi wake.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mukhtasari wa kile kilichomo kwenye ripoti yake ya ukaguzi wa mwaka 2017/18, CAG amesema kwamba kiasi cha fedha cha shilingi bilioni 3.74 za wanachama wake.
Mbali na Chama Cha Mapinduzi, CAG ameeleza kwamba, "Tumebaini CHADEMA ilinunua gari jipya aina ya 'Nisan Patrol' kwa Sh milioni 147.5 lakini lililisajiliwa kwa jina la mwanachama badala ya Bodi ya Wadhamini.
Ameongeza kwamba gari hilo kwenye taarifa ya fedha ilioneshwa kwamba kama mkopo kwa mwanachama huyo bila kuwa na makubaliano ya mkopo yaliyosainiwa kati ya mwanachama huyo na bodi ya wadhamini wa CHADEMA.
Mbali na CHADEMA, CAG amesema kwamba pia wamebaini kuwa majengo ya ofisi za CUF yamesajiliwa kwa majina ya watu badala ya Bodi ya Wadhamini.
Mbali n ripoti ya vyama, CAG amesema katika ukaguzi wamebaini kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilinunua mashine za BVR 8000 kwa ajili ya usajili wa wapiga kura, mashine 5000 hazikukidhi vigezo na hivyo kutolandana kimatumizi na zile zilizonunuliwa awali na NIDA na RITA na kusababisha hasara ya Sh862.08m.
Hata hivyo ukaguzi wa CAG umebaini kwamba katika ukaguzi maalumu uliofanywa katika ununuzi wa sare za askari polisi uliofanywa na Jeshi la Polisi nchini, na kwamba walibaini kwamba jeshi lililipa Sh16.66 bn bila kuwepo kwa ushahidi wa uagizaji wala upokeaji wa sare hizo.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
