Mwanaharakati, Alaa Salah (22) wa Sudan aliyeongoza maandamano ya kumtoa madarakani Rais wa nchi hiyo, Omar Al-Bashir ameonyesha furaha ya matunda ya kazi waliyoanza kuifanya tangu Jumatatu kwa kusema Bashir ameondoka.
Salah amejizolea umaarufu kwa picha yake ambayo amesimama juu ya gari katikati ya watu kusambaa sehemu nyingi ulimwenguni akitambulika kama shujaa kwa taifa hilo.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Salah ameandika kwamba, "Al-Bashir ameondoka, tumefanikiwa", ikiwa ni saa moja tangu Jeshi kuwaweka chini ya ulinzi viongozi waandamizi wa serikali ya Al - Bashir.
Mapema leo, kabla ya Shirika la Habari nchini Sudan kuhabarisha kwamba Jeshi la nchi hiyo linatarajia kutangaza taarifa muhimu juu ya mustakabali wa nchi, Salah aliweka wazi kwamba amekuwa akipokea vitisho vya kuuliwa baada ya picha na video zake kusambaa.
"Nimekuwa nikipokea vitisho vya kifo baada ya picha yangu & kusambaa . Sitamtukuza. Sauti yangu haiwezi kufutwa. Al-Bashir atawajibika ikiwa kitu chochote kitatokea kwangu," Salah.
Maandamano dhidi ya Bashir yalianza toka mwezi Disemba ambapo awali maandano yalianza kwa kupinga kupanda kwa bei ya vyakula lakini yamekuwa makubwa na kubadili lengo na kutaka kumng'oa rais madarakani.
Mpaka sasa Waziri Mstaafu wa Ulinzi, Abd al-Rahim Hussein na Waziri wa Ulinzi Awad Ibn Awaf wameripotiwa kukamatwa.
Salah ni mwanafunzi wa Chuo cha Kimataifa cha Sudan ambapo anasomea Uhandisi na usanifu.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
