Friday, March 22, 2019
Wanafunzi wa kike walia na wadau binafsi
Na. Rahel Nyabali,Tabora
Baadhi ya wanafunzi wa kike walio katika mpango wa TASSAF kwa lengo la kunusuru kaya masikini unaoratibiwa na mfuko wa maendeleo ya jamii wamewaomba wadau binafsi, kushirikiana na serikali ili kuweza kuwasaidia kutimiza malendo yao.
Muungwana Blog ilifika katika baadhi ya shule hapa mjini Tabora ikiwemo shule ya sekondari Kazehili na kuzungumzana na baadhi ya wanafunzi walio katika mpango wa TASSAF ili kujua maendeleo yao kitaaluma.
Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Kazehii Marium Seif amesema wanafunzi wa kike walikuwa wanashindwa kuhudhuria darasani kutokana na kukosa mahitaji muhimu ya shule ikiwemo madaftari na sare za shule
"Mpango huu wa TASSAF umetusaidia kwa kiasi kwa sababu zamani nilikua nakuja malamoja moja kwa wiki lakini baada ya kuwa katika mpango huu nahudhulia vizuri darasani ninawaomba wadau wengine wajitokeze kutusaidi," Amesema Marium.
"Mwalimu mlezi wa wanafunzi katika shule ya sekondari Kazehili Sarah Misa amesema wa wanafunzi walio katika mpango wa TASSAF amesema mpango huu umekuwa na tija kwa kwa kuongeza ufauru hasa kwa wanafunzi wa kike."
"Tuna wanafunzi kama mia moja wanahudhuria katika shule yetu baada ya kuwa katika mpango huu wanafunzi wanahudhulia kwa asilimia tisini hakika hili ni jambo kubwa,"amesema Sarah.
Aidha mpango huu umejikita zaidi katika kusaidia kaya masikini pamoja na watoto wanao ishi katika mazingira magumu ikiwemo Afya na Elimu ili kutimiza Malengo yao.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...