Sunday, March 24, 2019
Taarifa kwa Umma kutoka kwa SUMAJKT
Wabia wa Kampuni ya SUMAJKT Skyzone jana wamekagua eneo la Kiwanda cha taa za LED (Light Emitting Diode) kinachoendelea kujengwa chenye thamani ya zaidi shilingi za kitanzania bilioni 12 kinachojengwa katika Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa Mlalakuwa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea kuona hatua za utekelezaji wa Ujenzi wa Kiwanda hicho, Makamu wa Rais wa kampuni ya Everlight Skyzone ya nchini China, Bw. Hassan Baalbaki ambaye ni mmoja wa wabia wa SUMAJKT Skyzone amesema kiwanda hicho kinachojengwa kitatumia teknolojia mpya ambayo bado haijaenea nchi nyingi za Afrika.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Rajabu Mabele ambae ni mmoja wa wabia wa SUMAJKT Skyzone, amefafanua faida za kuwepo kwa kampuni hiyo hapa nchini, kuwa itasaidia kutatua changamoto ya upatikanaji wa taa hizo ambazo kwa sasa zinaagizwa toka nje ya nchi.
Kampuni hiyo ya ubia imeanzisha kiwanda hicho ambacho kitasaidia utekelezaji wa kauli mbiu ya Mh. Rais ya Tanzania ya viwanda na kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.
Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Everlight Skyzone Tanzania Bw. Victor Madata amesema katika kuunga mkono juhudi za Mh. Rais Dkt John Magufuli juu ya adhma yake ya Tanzania ya Viwanda, watafanya mafunzo kwa watanzania ili kutoa fursa za ajira na ujuzi wa jinsi yakutengeneza taa hizo na kuziuza nje ya nchi.
Kuanzishwa kwa kiwanda hicho kitaendelea kutekeleza kifungu cha 7 cha sheria ya uratibu wa Ajira kwa wageni kinachomtaka kila mwajiri kuandaa mpango wa urithishaji wa ujuzi kwa wafanyakazi Watanzania kwa lengo la kuhakikisha Watanzania wananufaika na ujuzi huo.
SUMAJKT Skyzone ni kampuni ya ubia kati ya SUMAJKT inayomiliki 49% na Everlight Skyzone inayomiliki 51% iliyoanzishwa mwezi Octoba 2018, Inatarajia kumaliza ujenzi huo mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu na kuanza uzalishaji wa taa hizo mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
