Sunday, March 24, 2019
Taarifa kwa Umma kutoka kwa SUMAJKT
Wabia wa Kampuni ya SUMAJKT Skyzone jana wamekagua eneo la Kiwanda cha taa za LED (Light Emitting Diode) kinachoendelea kujengwa chenye thamani ya zaidi shilingi za kitanzania bilioni 12 kinachojengwa katika Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa Mlalakuwa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea kuona hatua za utekelezaji wa Ujenzi wa Kiwanda hicho, Makamu wa Rais wa kampuni ya Everlight Skyzone ya nchini China, Bw. Hassan Baalbaki ambaye ni mmoja wa wabia wa SUMAJKT Skyzone amesema kiwanda hicho kinachojengwa kitatumia teknolojia mpya ambayo bado haijaenea nchi nyingi za Afrika.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Rajabu Mabele ambae ni mmoja wa wabia wa SUMAJKT Skyzone, amefafanua faida za kuwepo kwa kampuni hiyo hapa nchini, kuwa itasaidia kutatua changamoto ya upatikanaji wa taa hizo ambazo kwa sasa zinaagizwa toka nje ya nchi.
Kampuni hiyo ya ubia imeanzisha kiwanda hicho ambacho kitasaidia utekelezaji wa kauli mbiu ya Mh. Rais ya Tanzania ya viwanda na kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.
Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Everlight Skyzone Tanzania Bw. Victor Madata amesema katika kuunga mkono juhudi za Mh. Rais Dkt John Magufuli juu ya adhma yake ya Tanzania ya Viwanda, watafanya mafunzo kwa watanzania ili kutoa fursa za ajira na ujuzi wa jinsi yakutengeneza taa hizo na kuziuza nje ya nchi.
Kuanzishwa kwa kiwanda hicho kitaendelea kutekeleza kifungu cha 7 cha sheria ya uratibu wa Ajira kwa wageni kinachomtaka kila mwajiri kuandaa mpango wa urithishaji wa ujuzi kwa wafanyakazi Watanzania kwa lengo la kuhakikisha Watanzania wananufaika na ujuzi huo.
SUMAJKT Skyzone ni kampuni ya ubia kati ya SUMAJKT inayomiliki 49% na Everlight Skyzone inayomiliki 51% iliyoanzishwa mwezi Octoba 2018, Inatarajia kumaliza ujenzi huo mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu na kuanza uzalishaji wa taa hizo mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...