Saturday, February 9, 2019
Mollel Adai Kushambuliwa Lissu Kwa Risasi ni Mpango wa Chadema
Sakata la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kushambuliwa kwa risasi limeendelea kuzua matamshi na mitazamo mbalimbali ambapo leo, Mbunge wa Siha, Dkt. Godwin Mollel (CCM) amesema kuwa ulikuwa mpango wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Dkt. Mollel ambaye alikuwa mbunge wa Chadema na baadaye kuhamia CCM ambako aligombea tena na kurejea bungeni akiwa amebadili chama, ameliambia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa yeye aliiba sampuli ambazo chama hicho kilimkataza kuzitumia.
Mbunge huyo amedai kuwa alipojaribu kuwasilisha sampuli hizo ili zipelekwe Afrika Kusini kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi alikataliwa na uongozi wa chama hicho kikuu cha upinzani kwa kile alichodai walifahamu kuwa wangeumbuka.
"Mimi nilikuwa huko lakini nilikimbia kwa mipango yao, hata katika tukio la kushambuliwa Lissu mimi niliingia ndani kwenye uchunguzi na niliiba baadhi ya vitu lakini walikataa mapendekezo yangu," alisema Mollel.
Hata hivyo, wabunge wa Chadema, Frank Mwakajoka (Tunduma) na Joseph Selasini (Rombo), kwa nyakati tofauti waliomba kutoa taarifa kuhusu hoja ya Mollel ambapo walimtaka mbunge huyo kuthibitisha kauli zake na kutovunja kiapo chake cha udaktari.
Akijibu kuhusu taarifa hiyo, Dkt. Mollel alidai kuwa ili athibitishe anataka Chadema waeleze wanakopeleka ruzuku za chama hicho pamoja na kile alichodai kuwa ni mpango wao dhidi ya Zitto Kabwe na marehemu Chacha Wangwe walipojaribu kugombea uenyekiti wa chama hicho.
Lissu amekuwa mjadala kwa nyakati tofauti ndani ya Bunge wiki hii kutokana na kauli anazozitoa hivi karibuni katika ziara zake za ughaibuni. Spika wa Bunge ameahidi kufanyia kazi hoja iliyowasilishwa na Mbunge wa Geita, Joseph 'Msukuma' Kasheku kuwa ofisi ya Bunge isitishe mshahara na stahiki za Lissu.
Mbunge huyo wa Singida Mashariki jana aliiambia Sauti ya Amerika kuwa anaendelea na matibabu na anatarajia kufanyiwa upasuaji wa 23 nchini Ubelgiji.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
