Mtoto aliyejulikana kwa jina la Meshack Myonga mwenye umri wa miaka 4 mkazi wa Mji Mwema mkoani Njombe ambaye alijeruhiwa kwa kukatwa koromeo amefariki dunia mwishoni mwa juma hili akiwa katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya alipolazwa lwa ajili ya matibabu.
Mtoto huyo ambaye aliokotwa barabarani jirani na pori akiwa amejeruhiwa kwa kukatwa koromeo Desemba 23, 2019 majira ya saa 4 asubuhi mtaa wa Mji Mwema.
Akizungumza kwenye mazishi ya mtoto huyo jana katika kijiji cha Ngalanga Mjini Njombe, mjomba wa marehemu Gisbeth Mlelwa, amesema mtoto huyo alizidiwa kwa majeraha makali tangu alipovamiwa na watu wasiojulikana.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtaa huo, Alanus Mwalongo ameonesha kusikitishwa na tukio la kifo cha mtoto huyo na kueleza kuwa jambo hilo linapaswa kupingwa na kila mmoja.
Hivi karibuni, Mkuu wa Operesheni za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna Liberatus Sabas, na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Renata Mzinga wameanzisha zoezi la kuwasaka wahalifu wa matukio ya mauaji ya watoto ambapo walikagua mapori ya Nundu na Tanwat mkoani Njombe.
Source
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
