Sunday, September 9, 2018
Dk Ndugulile awaasa wananchi kutoa taarifa wanapokosa matibabu
Na.Ahmad Mmow, Nachingwea.\
NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto ,Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) amewaasa wananchi kutoa taarifa pale watakapokwenda hospitali na kukosa matibabu kwasababu ya kukosekana dawa.
Ndugulile ametoa rai hiyo jana katika kijiji cha Naipanga,wilaya ya Nachingwea wakati wa kilele cha kampeni ya kupima kwa hiyari maambukizi ya virusi vya UKIMWI ambayo imepewà na kutambulika kwa jina la "Furaha Yangu ".
Aliwahakikishia wananchi hao na wengine wote hapa nchini kwamba serikali ya awamu ya tano haitaki kuona wananchi wakienda kununua dawa madukani hivyo imejipanga kuhakikisha dawa zote zinazotolewa na serikali zinawafikia.
Alisema katika kuhakikisha huduma za afya zinatolewa kwa wananchi Serikali imewapeleka watumishi wa idara ya afya 48 katika wilaya hiyo ili wakatoe huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya vilivyopo wilayani humu.
"Upimaji wa virusi vya UKIMWI ni mpango wa kitaifa ili kuhakikisha kila Mtanzania anapima na kutambua afya yake, lengo ni kuwafikia asilimia 90 ya watu walioambukizwa na kutoa dawa,"alisema DkNdugulile ambae pia ni mbunge wa jimbo la Kigamboni.
Kwa upande wake ,mkuu wa wilaya Nachingwea, Rukia Muwango alisema zoezi la upimaji afya katika wilaya hiyo ni endelevu, kwani umuhimu wa wananchi kupima na kutambua afya zao ni mkubwa huku akiweka wazi kwamba maendeleo yatatokana na uimara wa afya za wananchi kwasababu mtaji wa kwanza wa maendeleo na uchumi wa taifa ni afya.
Mkuu huyo wa wilaya alibainisha kwamba kampeni hiyo ya upimaji kwa hiari inayoendelea wilayani humo ambayo yeye kwa kushirikiana na watalaam wa idara ya afya anaratibu na kusimamia.Tayari wanawake 809 na wanaume 531wamejitokeza na kupimwa.
"Hadi sasa miongoni mwahao waliopima ni watu saba tu ndio waliokutwa na maambukizi ya VVU na wameshapata ushauri nasaha na kuanzishiwa dawa za kupunguza makali ya Virusi Vya UKIMWI,"alisema Muwango.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
