Mzozo wa kidiplomasia unazidi kuibuka kuhusu nchi ndogo iliyo kusini mwa Afrika ya eSwatini ambayo awali ilifahamika kama Swaziland.
Nchi hiyo ndiyo mshirika wa mwisho wa Taiwan aliyesalia barani Afrika.
China ambayo hairuhusu nchi yoyote kuwa na uhusiano wa kiserikali nayo pamoja na Taiwan kwa wakati mmoja imesema inataka eSwatini kuboresha uhusiano kati yake na Beijing.
Taiwan ambayo China inaitaja kuwa mkoa wake, imekuwa ikipoteza washirika wakiwa sasa wamebaki 17 tu. Siku ya Jumanne El Salvador ilikata uhusiano wake na China.
Taiwan iliapa Jumanne kupambana na tabia za China baada ya kupoteza mshirika wake El Salvador kwa China, ambayo ni nchi ya tatu kukata uhusiano wake na Taiwan na kujiunga na China mwaka huu.
"eSwatini haina uhusianoa na China kwa sababu ambazo kila mtu anazifahamu," naibu waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa China Cheng Xiaodong aliliambia shirika la habari la Reuters.
"Tuna matumaini kuwa nchi zote za Afrika huku moja ikiwa imebaki, zitashiriki katika kuwa na uhusiano mzuri kati ya China na Afrika," alisema.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
