Mzozo wa kidiplomasia unazidi kuibuka kuhusu nchi ndogo iliyo kusini mwa Afrika ya eSwatini ambayo awali ilifahamika kama Swaziland.
Nchi hiyo ndiyo mshirika wa mwisho wa Taiwan aliyesalia barani Afrika.
China ambayo hairuhusu nchi yoyote kuwa na uhusiano wa kiserikali nayo pamoja na Taiwan kwa wakati mmoja imesema inataka eSwatini kuboresha uhusiano kati yake na Beijing.
Taiwan ambayo China inaitaja kuwa mkoa wake, imekuwa ikipoteza washirika wakiwa sasa wamebaki 17 tu. Siku ya Jumanne El Salvador ilikata uhusiano wake na China.
Taiwan iliapa Jumanne kupambana na tabia za China baada ya kupoteza mshirika wake El Salvador kwa China, ambayo ni nchi ya tatu kukata uhusiano wake na Taiwan na kujiunga na China mwaka huu.
"eSwatini haina uhusianoa na China kwa sababu ambazo kila mtu anazifahamu," naibu waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa China Cheng Xiaodong aliliambia shirika la habari la Reuters.
"Tuna matumaini kuwa nchi zote za Afrika huku moja ikiwa imebaki, zitashiriki katika kuwa na uhusiano mzuri kati ya China na Afrika," alisema.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...