Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira imeitaka serikali kukaa na wamiliki wa viwanda nchini na kuhakiki gharama za uzalishaji ambazo zimekuwa zikisababisha bidhaa za wazalishaji wa ndani kushindwa kushindana na zinazoingizwa nchini.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Sadick Murad ametoa kauli hiyo jana Agosti 13, wakati kamati hiyo ilipotembelea kiwanda cha uzalishaji wa mabati na vifaa vingine Alaf.
Murad amesema gharama za uzalisha zimekuwa kikwazo kwa viwanda vya ndani ambazo vinazalisha bidhaa kwa bei ghali ilihali zinazoingizwa nchini zinauzwa kwa bei rahisi.
"Gharama za uzalisha zikiwa fair na wazalishaji wa ndani kupunguziwa kodi za umeme na tozo nyingine, gharama za uzalishaji zitashuka," amesema ambaye pia ni Mbunge wa Mvomero (CCM).
Aidha, alitoa wito kwa wizara ya viwanda, biashara na uwekezaji, kuisimamia vema Shirika la Viwango (TBS) na Mamlaka ya Mapato (TRA) ili ziendelee kutoa huduma rafiki kwa wazalishaji wa ndani ambao wamekuwa chachu katika uzalishaji wa ajira na ukuzajia uchumi.
Hata hivyo, Katibu mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Profesa Joseph Buchweshaija amesema tayari imeandaa mpango maalumu wa kwa kushirikiana na TBS kuondoa bidhaa hafifu sokoni. Tayari tumeanza kuisafisha suala hilo na ninawaahidi kuendelea kutekeleza yote mliyoagiza," amesema.
Aidha, Meneja Mkuu wa kiwanda hicho cha Alaf, Dipti Mohanty aliieleza kamati hiyo kuwa umeme umeendelea kuwa mojawapo ya kikwazo kikubwa katika uzalishaji wa bidhaa zao.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Mamlaka za China zipo mbioni kudhibiti ongezeko la harusi za kifahari amabazo zimekuwa zikishamiri katika miaka ya karibuni. Kwamujibu wa ma...