Wednesday, May 27, 2020
Maskini Juma Pondamali KOCHA wa Makipa Aishtaki Young Africans
Aliyekua kocha wa makipa Young Africans Juma Pondamali amelazimika kuishtaki klabu hiyo kwa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), kushinikiza kulipwa mshahara wake wa miezi saba.
Pondamali ambaye ni mlinda mlango wa zamani wa klabu hiyo kongwe nchini, alitimuliwa mwaka jana baada ya klabu hiyo kuvunja benchi lote la ufundi lililokuwa chini ya kocha Mwinyi Zahera.
Kocha huyo anayeinoa African Sports kwa sasa, amesema kuwa baada ya kuona hakuna dalili za kulipwa madeni yake, ameamua kupeleka suala hilo TFF anakoamini atapata haki yake.
"Wakati tunaondolewa nilikuwa nikidai mshahara wa miezi saba, uongozi ulisema utanilipa ndani ya muda mfupi lakini imekuwa tofauti na makubaliano," amesema Pondamali.
Amesema kabla ya uchaguzi mkuu wa mwisho kufanyika kwenye klabu ya Young Africans walifanya kazi katika mazingira magumu ikiwamo kutolipwa mshahara kwa miezi hiyo saba.
"Klabu ilikuwa kwenye hali ngumu na tulifanya kazi kwa mazingira hayo hayo, tukiamini uongozi mpya ukiingia madarakani utatulipa, lakini ikawa tofauti, tukaishia kuondolewa.
"Tuliambiwa baada ya siku chache tutalipwa fedha zetu, lakini imekuwa ndivyo sivyo na binafsi nimeona sina njia nyingine ya kupata haki yangu zaidi ya kwenda kushtaki TFF," anasema.
Mwenyekiti wa Young Africans, Dk Mshindo Msolla alikiri klabu hiyo kudaiwa.
"Si Pondamali pekee ambaye anatudai, klabu inadaiwa na watu mbalimbali na madeni yote tunayatambua na tutayalipa," anasema Dk Msolla.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
