Mtafiti wa Chuo kikuu cha Makerere nchini Uganda Dkt. Stella Nyanzi ameagizwa kujitetea katika kesi ambapo anatuhumiwa kumtukana rais Yoweri Museveni.
Ikitoa uamuzi wake mahakama iliopo katika barabara ya Baganda ilisema kuwa alikuwa na kesi ya kujibu.
Kwa mujibu wa gazeti la The Monitor nchini Uganda, baada ya kusikiza ushahidi kutoka kwa mashahidi watatu wa serikali, hakimu bi Gladys Kamasanyu aliamuru siku ya ijumaa kwamba Dkt Nyanzi, ambaye anazuiliwa katika gereza la Luzira ana kesi ya kujibu.
Baada ya uamuzi huo Dkt Nyanzi alisema kuwa atawasilisha kati ya mashahidi watano hadi saba kumtetea.
Hakimu huyo amesema kuwa mshukiwa huyo anamiliki akaunti ya ukurusa wa facebook ambao ulichapisha 'matusi' hayo.
Dkt Nyanzi anashtakiwa kwa kutekeleza unyanyasaji wa mtandaoni pamoja na kutoa matamshi machafu swala ambalo linakiuka sheria nchini Uganda.
Mnamo tarehe 9 mwezi Novemba , Dkt Nyanzi alikataa kuomba dhamana.
Hatahivyo bwana Isaac Ssemakade, wakati huo alisema kwamba mteja wake alitaka serikali kuharakisha uchunguzi ili kumwezesha kuendelea na kesi.
Upande wa mashtaka unasema kuwa mnamo mwezi Septemba tarehe 16 2018, Dkt Stella Nyanzi alichapisha katika ukurasa wake wa facebook madai yaliodaiwa kuwa machafu kwa rais Museveni na marehemu mamake.
Imedaiwa kwamba pia alichapisha ujumbe wa kuvuruga amani, utulivu na kuingilia faragha ya rais Museveni.
Hii ni mara ya pili maafisa wa polisi wanamtuhumu Dkt Nyanzi kwa madai ya kumtusi Museveni na familia yake.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
