Thursday, June 20, 2019
Hatuna nia ya kuwakomoa wananchi - Mkurugenzi wa BAWASA
Na John Walter-Babati .
Mkurungenzi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira Babati (BAWASA) Idd Msuya amewataka wananchi kuacha kulalamika kuhusu kupanda kwa bei ya maji kwa unit kutokana na uhitaji mkubwa wa fedha za kuendelea kushughulikia miradi mingine ya maji kwenye sehemu ambazo zina uhaba wa maji.
Akiongea na waandishi wa Habari ofisini kwake mtaa wa Miomboni Mjini Babati, Mkurugenzi Mtendaji wa BAWASA Mhandisi Iddy Msuya alisema kuwa ongezeko hilo la asilimia 36 ni sawa na bei ya shilingi 1,748 kwa unit moja ya maji, bei ambayo ni ndogo ukilinganisha na mikoa mingine.
"Sisi kama BAWASA lengo letu la kupandisha bei ya maji hatuna nia ya kuwakomoa wananchi wetu hapana hii ni kuweza kupata fedha za kuweza kukarabati miundombinu ya maji ili ile kero ya kukatika kwa maji ifutike kabisa ili hata mtu akiamka usiku wa manane akifungulia maji yanatoka.
"Bei ya maji katika mkoa wa Arusha wenye chanzo cha maji ya mtiririko ni Shilingi 1,500 kwa unit moja sawa na asilima 50 ya ongezeko la bei ya maji hivyo Babati bado iko vizuri" Alisema Msuya.
Kwa mujibu wake hali ya upotevu wa maji imepungua na kufikia asilimia 35 kutokana na juhudi ya mamlaka ya BAWASA kuboresha miundo mbinu ya mabomba ya zamani ambayo baadhi yao iliwekwa katika kipindi cha Uhuru ambayo imechoka na kupoteza maji mengi.
Alisema kwa utaratibu BAWASA inapotaka kuongeza bei ya maji kwa walaji wake huomba mapendekezo ya ongezeko hilo la maji EWURA ambao huchukua mapendekezo kutoka kwa wadau na kuyapeleka Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa ajili ya kutoa kibali cha ongezeko hilo.
Mhandisi Msuya alifafanua kuwa BAWASA walipendekeza kuongeza bei kwa shilingi 2,175 kutokana na gharama za uendeshaji lakini baada ya kukusanya maoni ya Walaji na EWURA bei pendekezwa ilikuwa ni Shilingi 1,748 bei ambayo haikufanikiwa.
Msuya alibainisha kuwa kupanda kwa bei ya maji huwa inatolewa maelekezo mfano kununua mita za maji zipatazo 5,000, kuongeza mitandao ya maji kutoka Ng'wang'warai kuelekea shue ya msingi Tarangire na kujenga machujio ya maji ya kijiji hicho na Mutuka.
hata hivyo alisema ni azma ya serikali ya kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2020 upatikanaji wa maji ufikie asilimia 100 kwa wananchi waishio vijijini na kwamba BAWASA imejiwekea lengo la kuhakikisha wakazi wake wanapata maji kwa uhakika bila mgao au kulazimika kuchota maji.
Baadhi ya wananchi wa mji wa Babati walisema BAWASA haijawatendea haki kwani hawakushirikishwa kuongezeka kwa bei ya maji huku huduma ikiwa hairidhishi kwani hakuna mabadiliko ya huduma kwa kuwa maji yanayotoka ni machafu.
"Maji yanayotoka na ndio tunayoyatumia kwa kunywa, tunakunywa maji machafu sana wametupandishia bei ya maji lakini huduma ndo imezidi kuwa mbaya zaidi, maji yanatoka machafu na tulishawaambia wakasema watafuatilia lakini hadi leo kimya watatusababishia tuumwe matumbo," Alisema Yusufu Mdoe.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...