MAPOROMOKO ya udongo yaliyotokana na mvua kubwa yamesababisha vifo vya watu 60 katika mikoa ya Durban na KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini.
Zaidi ya watu 1,000 wameondoka kutoka makazi yao kwa mujibu wa Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ambaye ametembelea maeneo yaliyoathiriwa.
Mvua kubwa imekuwa ikinyesha katika maeneo ya kusini na mashariki mwa nchi hiyo siku chache zilizopita. Mafuriko zaidi na upepo mkali unatarajiwa katika maeneo ya pwani huku onyo likitolewa kuhusu hali mbaya ya hewa.
Mafuriko hayo makubwa yaliharibu biashara na nyumba za watu na vyuo vikuu viwili – huku mamia ya watu wakiondoka katika makazi yao.
Ramaphosa amezitembelea familia zilizopoteza wapendwa wao katika mafuriko hayo. Mwandishi wa BBC Nomsa Maseko amesema kuwa rais aliweka shada la maua katika eneo ambalo watu wanane walifariki.
Pia alionekana akiwasukuma walinzi waliokuwa wakiwazuia watu kusema naye.
"Ni muhimu kuja kuona kile kilichofanyika au kilichotokea na kuomboleza na familia zilizopoteza wapendwa wao katika janga hili. Kupoteza maisha sio jambo rahisi, hasa maafa yakitokea ghafla," alisema Ramaphosa.
Wakati hayo yakijiri, Waziri wa Tawala za Mikoa, Nomusa Dube-Ncube, amewaambia maofisa wa kituo cha radio cha SAFM kwamba bado wanaendelea kutathmini kiwango cha uharibifu uliosababishwa na mkasa huo, kwa mujibu wa shirika la habari la AFP.
Siku zijazo watu watalazimika kuhamishwa kutoka maeneo yaliyoathirika, alisema. Watu kadhaa wamepelekwa hospitali huku shughuli ya kuwatafuta manusura waliyozikwa chini ya vifusi vya majengo yalioporomoka.
Source
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
