TAARIFA NA SALAAM ZA POLE MSIBA WA MAMA MZAZI WA MZEE SUMAYE
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa masikitiko na majonzi makubwa taarifa za Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama na Waziri Mkuu Mstaafu, Mzee Frederick Sumaye kupata msiba wa kufiwa na Mama yake Mzazi, Bi. Elizabeth Gisa Sumaye, aliyefariki Jumatano, Novemba 7, 2018 kijijini kwake Endasaki, Hanang, mkoani Manyara kwa ugonjwa wa moyo na mapafu.
Kufuatia msiba huo, CHADEMA kupitia Katibu Mkuu wa Chama, kinatoa salaam za pole na rambirambi kwa Familia ya Mzee Sumaye, ndugu na jamaa kwa kufiwa na Mama na Bibi, akiwa ni moja ya nguzo muhimu katika familia na maisha yao. Mwenyezi Mungu awapatie faraja na kuwajalia nguvu wakati huu wa majonzi makubwa ya kuomboleza msiba huo.
Chama kitaendelea kushirikiana na Familia ya Mzee Sumaye kutoa taarifa kuhusu msiba huo ambao shughuli zake, ikiwemo mazishi, zitafanyikia kijijini Endasaki, Hanang, Manyara.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
