Tuesday, September 24, 2019

Waziri Jafo awataka Watanzania kujitokeza Tamasha la JAMAFEST


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Suleiman Jaffo, amewataka watanzania
kujitokeza kwa wingi katika tamasha la JAMAFEST linaloendelea katika Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam ili kujifunza Utamaduni wa nchi zinazoshiriki tamasha hilo.

Waziri Jaffo ameyasema hayo mapema hii leo alipotembelea maonesho ya Utamaduni wa Nchi za Afrika Mashariki yanayoendelea katika uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.

"Naomba nitumie nafasi hii kuwaomba watanzania kujitokeza kwa wingi katika
tamasha hili la Utamaduni ili kujifunza Utamaduni wa nchi mbalimbali zinazoshiriki
tamasha hili na hii ndio fursa pekee ya kukuza lugha ya Kiswahili ili kuunga mkono
juhudi za Mheshimiwa Rais," Waziri Jaffo.

Aidha Waziri Jaffo amewakumbusha amesema kuwa tamasha hili ni la kihistoria hapa nchini kwani limekutanisha zenye Utamaduni tofautitofauti kwa wakati mmoja hivyo ni fursa kwa watanzania kujifunza mambo mbalimbali kama ususi, ushonaji, ngoma za asili na michezo mbalimbali.

Tamasha la JAMAFEST linashirikisha jumla ya nchi tano ambazo ni Kenya, Uganda,
Burundi, Rwanda na wenyeji Tanzania tamasha hilo linarajiwa kumalizika siku ya
tarehe 28 Septemba 2019

Saturday, September 21, 2019

Kilimo bora cha maboga


Boga ni zao ambalo mmea wake unakuwa kwa kutambaa na ni la mviringo, ngozi yake ni nyororo na rangi yake ni ya njano inayoelekea kwenye rangi ya chungwa au rangi ya kijani. Katikati ya boga kuna mbegu na massa, Boga lipo katika jamii ya Cucurbita pepo.

Asili yake
Asili ya boga ni Amerika kaskazini, maboga yamekuwa yakipandwa kwaajili ya biashara na kwaajili ya chakula. Kwa sasa maboga yamekuwa yakilimwa maeneo mbalimbali duniani, Antarctika pekee ndiko maboga hayawezi kustawi. Mataifa yanayozalisha maboga kwa wingi ni Marekani (USA), Canada, Mexico, India, and China.

Hali ya hewa & udongo 
Maboga yanahitaji joto la wastani kutoka kwenye jua, pia eneo ambalo halituamishi maji udongo wake uwe na pH kati ya 6.0 – 6.8. Pia udongo uwe na joto inchi tatu (sm 7.6) kushuka chini angalau nyuzi 60 °F (15.5 °C), maboga yatadhoofika kama maji yatakosekana.

Utayarishaji wa shamba
Shamba litayalishwe kwa umakini bila kuwa na sehemu ya kutuamisha maji maana mmea wa maboga na maboga yenyewe hutambaa chini, tumia jembe la ng'ombe, trekta, jembe la mkono au pawatila, changanyia mbolea za asili (samadi au mboji) na udongo ili kurutubisha shamba.

Utayarishaji wa mbegu
Mbegu za maboga zinatoka ndani ya maboga, kuna mbegu zilizoboreshwa (za kisasa) na za asili, andaa mbegu mapema wiki moja au mbili kabla ya kupanda.

Upandaji
Maboga hupandwa kwa kufukia mbegu sentimita 1 au 2 chini ya udongo , panda mbegu 2 kila shimo. Pia panda umbali wa sentimeta 30 kutoka shina hadi shina na mita 1.5 – 2 kutoka mstari hadi mstari.

Matandazo (mulches )
Kwasababu ni zao linalotambaa basi lazima tuangalie namna ya kutandaza, weka nyasi na mabaki ya mimea mingne kufunika ardhi. Baada ya miche kutambaaa kwa kiasi unaweza kuweka matandazo (mulches) ambayo yaweza kuwa nyasi kavu kwenye udongo ili kuzuia upotevu wa unyevu vile vile kupunguza uotaji wa magugu shambani kwako. Vile vile matandazo yakioza yanaongeza rutuba kwenye udongo na hulinda udongo dhidi ya mmomonyoko wa udongo.

Mbolea
Katika matumizi ya mbolea yanatofautiana kutokana na mbegu, Lakini tumia mbolea za asili (samadi au mboji) ili kuongeza rutuba kwenye udongo, ukihitaji kutumia mbolea za viwandani weka kiasi sana, labda eneo hilo kama hakuna rutuba, mbolea ya NPK inaweza tumia.

Upaliliaji & unyevu
Palilia shamba nyasi zinapoanza kuota, pia safisha shamba ili kuondoa wadudu. Shamba la maboga linatakiwa liwe na unyevunyevu kila mara ili maboga yaweze kustawi vizuri yasidumae.

Uvunaji
Maboga hukomaa baada ya siku 95 mpaka 120, ili kujua kuwa boga lako limekomaa unaangalia kikonyo, kikonyo cha boga kinapoteza maji na kinaanza kuwa kikavu.

Thursday, September 19, 2019

MAMBO Manne (4) Ya Kimafanikio Ya Kumfundisha Mtoto Wako Mapema...!!!


Msingi mkubwa wa mafanikio ya mtu yeyote kitabia unatokana na malezi bora aliyopata hasa akiwa mtoto kuanzia mwaka mmoja hadi miaka kumi na mbili. Katika kipindi cha mwaka 1 hadi 12 ndio kipindi muhimu sana cha malezi.

Tabia nyingi ambazo zinatengenezwa au kufundishwa katika kipindi hiki, huwa kuna uwezekano mkubwa wa kudumu maishani mwako kote. Hapa hii inatokea bila kujali tabia hiyo ni nzuri kwako au mbaya.

Kwa mfano, kama ulikuwa unaendekeza uvivu au kama ulikuwa mtu wa kuchapa kazi sana na kujiona huo ndio kama utamaduni katika kipindi cha mwaka 1 hadi 12, ni rahisi tu tabia hizo kuendelea hadi ukubwani.

Kwa mantiki hiyo ndiyo maana ni muhimu sana kumfundisha mtoto wako mambo ya kimafanikio yatakayomsaidia  kwa baadae kwenye maisha yake. Mambo hayo ni yepi? Karibu na twende pamoja tujifunze.   

1. Mfundishe, njia bora ya kufikiri.

Ikiwa hupendi sana maisha yako yalivyokuwa mwanzoni yaendelee kwa kizazi chako, sasa ni wakati wa kumfundisha mtoto wako namna bora ya kufikiri. Hapa ni lazima umfanye mtoto wako aweze kufikiri chanya.

Unaweza kumfanya moto wako afikiri chanya kwa kumpa vitabu vizuri chanya kama uwezo wa kusoma anao au kwa maneno maneno unayomwambia. Hiyo haitoshi pia unaweza ukamtafutia marafiki wazuri wenye mtazamo chanya.

Kama mtoto wako unamlea kwa mtazamo chanya, kufikiri kwa njia bora itakuwa kwake ni jambo ambalo halikwepeki. Anza leo kuweka mikakati yakumjengea mwanao njia bora ya kufikiri itakayomsaidia hata kumjengea mtazamo chanya pia.

2. Mfundishe, kujitegemee mapema.

Kati ya kitu kitakachofanya ujenge msingi imara kwa watoto wako kwa baadae ni kule kufanya wajitegemee mapema. Hapa inatakiwa umfundishe mtoto wako kufanya baadhi ya mambo mwenyewe.

Kwa mfano, anapokuwa mkubwa kidogo kama ni kufua mwache afue mwenyewe. Kama ni kusaidia kazi fulani acha aifanye. Njia hii inakuwa bora kwa kujua kwamba kuna vitu fulani anatakiwa awajibike.

Lakini kama utakuwa ni mtu wa kumlea mtoto wako kwa kutaka kila kitu  afanyiwe basi wewe ndiye utakuwa mtu wa kwanza kumharibu mtoto wako. Mfanye mtoto wako ajitegemee mapema, 
itamsaidia sana kwa baadae katika makuzi yake.

3. Mfundishe, ajifunze kuchukua hatua mapema.

Siku zote vitendo ni bora sana kuliko kusema. Kwa kuwa unajua umuhimu wa hili anza kumfundisha mtoto wako juu ya umuhimu wa kuchukua hatua mapema katika maisha yake hata kwa vitu vidogo ambavyo anavyofanya.

Kwa kumfundisha hivi unakuwa unajenga utamaduni imara ambao utamfanya mtoto wako hata atakapokuwa mkubwa atakuwa anajua na kutambua umuhimu wa kuchukua hatua mapema pia kwenye maisha yake.

Ili hili lifanikiwe, mfundishe kitu fulani halafu anza kufatilia utekelezaji. Unaweza ukamwacha hata maswali kama kazi ya nyumbani, halafu uone atamaliza baada ya muda gani? Utakuwa unafanya hivyo mara kwa mara ili kumfanya achukue hatua mapema zaidi.

4. Mfundishe ajue mambo yote huwa hayaendi kama yalivyopangwa.

Katika kumfundisha atambue kwamba mambo kuna wakati hayaendi kama yanavyopangwa, subiri kipindi ambapo anataka kitu fulani tena kwa hamu kubwa. Inapofika katika hicho kipindi kwa makusudi mnyime.

Najua kama ilivyo kwa watoto walio wengi tabia zao atalia. Mwache alie halafu tafuta siku ama muda akitulia, kama kile kitu kilikuwa cjha kununua, mnunulie na mpe somo mapema atambue kuna wakati mambo hayaendi moja kwa moja kama uliyopanga.

Fanya hivi kwa mtoto ambae ameshaanza kujitambua ikiwezekana kuanzia angalau darasa la tano. Rudia tena na tena zoezi hili, mpaka ifike mahali ajue kwamba mategemeo na uhalisia ni vitu viwili tofauti.

Yapo mambo mengi unayoweza kumfundisha mwanao ya kumweka juu kimafanikio kwa baadae. Unaweza kumfundisha mwanao pia jinsi ya kuishi na watu sahihi, uaminifu katika maisha, misingi bora ya kuishi maisha ya kiroho napengine hata faida ya kujiamini.

Fanyia kazi haya machache kwa leo na chukua hatua katika kuweza kufikia mafanikio yako makubwa.

Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
0713 04 80 35,

DC NYIMBI AZINDUA MBIO NDEFU ZA ROCK CITY MARATHON 2019 MWANZA

Na Fabian Fanuel - Malunde 1 blog
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza Dkt. Phillis Nyimbi leo amezindua mbio ndefu za Rock City Marathon 2019 katika Uwanja wa Rock City Mall Mwanza.

Uzinduzi huo umefanyika leo Alhamis Septemba 19,2019 ukishirikisha wadau mbalimbali wa mbio hizo, viongozi kutoka Serikalini, Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali, Wadhamini wa mbio pamoja na waandishi wa habari.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela, Mkuu wa wilaya ya Nyamagana  Dkt. Phillis Nyimbi amewashukuru waandaji wa mbio hizo 'Capital Plus International' kwa kazi kubwa wanayoifanya na kuomba washiriki wengi kujiandisha kwa mwaka huu kushiriki mbio hizo zitakazofanyika Mkoani Mwanza 20 Oktoba mwaka huu.

Huu ni msimu wa kumi wa mbio hizi ambazo zimekuwa na mwitikio mkubwa kutokana na washiriki wengi kuongezeka kila mwaka na mwaka huu inatarajiwa washiriki zaidi ya elfu tatu watashiriki huku waandaji wakiweka bayana zawadi zaidi ya Milioni 30 zitashindaniwa kwa mbio za Aina mbalimbali Kama kilomita 42, 21, 5 na 2.5.

Miongoni mwa wadhamini wa mbio ndefu za Rock City Marathon 2019 ni Tigo Rock City Mall,Tiper, Global Guard,Mwanza Water,Pigeon Hotel,Bodi ya Utalii na Pepsi.
Mkuu wa Mkoa wa Nyamagana Dr Phillis Nyimbi akisaini namba yake ya ushiriki wa mbio za Rock City Marathon huku Mratibu wa mbio hizo Magdalena Laizer na Katibu wa chama cha mbio Mkoa wa Mwanza Peter Mugaya wakishuhudia.


Msimamizi wa Mbio za Rock City Marathon John Bayo akimvisha Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi medali.
Msimamizi wa Mbio za Rock City Marathon John Bayo akimvisha Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi medali.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi akionesha medali.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi akionesha medali.

Mkuu w Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi akikata utepe wa Uzinduzi wa mbio za Rock City Marathon 2019 uliofanyia Viwanja vya Rock City Mall Mwanza.

Tuesday, September 17, 2019

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

Dalili:mwili kuchoka,maumivu ya mgongo na kiuno,kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu

Misuli  kulegea na kusinyaa hata kushindwa kufika kileleni miguu kuuma na kuwaka moto:

TIBA YAKE:

TULLO4 MIX.Ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizi hayo, inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kukufanya urudie tendo la ndoa zaidi mara tatu bila kuchoka au kukinai.

NTINJE3 PUMP.Ni dawa inayoongeza maumbile na kukupa umbile la kudumu.Itumie tiba hii kuokoa ndoa yako na kuokoa kukimbiwa na umpendae.
GASELA: Ni dawa mvuto kumvuta umpendae na kumrudisha alie mbali .

NTOBO: Inatibu KISUKARI:siku7 na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenyetatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari.

mpigie DR LIZENGO .OFISI IPO MBAGALA SABASABA.SIMU 0655283534/0621737576


Tuesday, September 10, 2019

Nyumba Inauzwa Ipo Dodoma Uzunguni Bei Chee Kabisa...



BEST DALALI anakutangazia kuna Nyumba inauzwa ipo Dodoma maeneo ya Uzunguni, Nyumba inaukubwa wa mita 51 kwa 28 sawa na Sq.m 1,428, Nyumba haina mgogoro ipo Full Document, Bei Milion 200, wasiliana nasi kwa maelezo zaidi. 0657 16 82 72 / 0689 95 33 35

Pia kama una Nyumba ya kupangisha au kuuza au Kiwanja au Shamba unataka kuuza au kununua usipate tabu BEST DALALI tupo kwa ajili yako.  piga simu kwa mawasiliano zaidi 0657 16 82 72 / 0689 95 33 35

Mikoa tunayo ihudumia ni Dar es salaam, Dodoma, Arusha na Mwanza


Friday, September 6, 2019

Kambi Ya Kitaaluma Kwa Wanafunzi Wa Kidato Cha Nne Wenye Ufaulu Hafifu Yazinduliwa Simiyu

Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amezindua rasmi kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wa kidato cha nne waliopata ufaulu hafifu (daraja sifuri) katika mtihani wa 'Mock', lengo likiwa ni kuwasaidia waweze kuongeza ufaulu wao katika mtihani wa Taifa utakaofanyika mwezi Novemba 2019.

Akizindua kambi hiyo Septemba 05, 2019 Mtaka amesema wanafunzi hao watafundishwa masomo manne tu ambayo ni Kiswahili, Kiingereza ,Uraia(Civics) na Historia, hivyo akatoa wito kwa walimu mahiri waliochaguliwa kuwafundisha wanafunzi hao kwa moyo na upendo ili wanafunzi hao waweze kupata alama D na kuendelea katika mtihani wa Taifa.

"Hawa watoto wafundisheni masomo manne, Kiswahili, Kiingereza, Historia na Civics; wafundisheni kwa moyo, wapeni mazoezi ya mara kwa mara katika siku hizi 60 watakazokuwa kambini, muwasaidie watoke kwenye F wapate angalau D nao wapate vyeti, kwa sababu hata ajira siku hizi kigezo ni angalau mtu awe na cheti cha kidato cha nne" alisema Mtaka.

Katika hatua nyingine Mtaka ametoa wito kwa jamii ya Simiyu kuendelea kuwekeza kwenye elimu ili kuuwezesha mkoa kushindana kiuchumi kwa kuwa maendeleo ya kiuchumi yanategemea maendeleo ya elimu katika eneo husika.

Afisa Elimu mkoa wa Simiyu, Mwl.Ernest Hinju amesema kati ya Wanafunzi 9956 waliofanya mtihani wa  Utimilifu (Mock), 1300 hawakupata alama D hata moja, hivyo waliopata matokeo hafifu (daraja sifuri) wamewekwa pamoja wafundishwe masomo manne ili waweze kuongeza ufaulu katika mtihani wa Taifa, huku waliopata daraja la kwanza hadi la nne wakiendelea na kambi kufundishwa masomo yote.

Aidha, Hinju ameongeza kuwa  kambi za kitaaluma zimechangia kuongeza ufaulu kwenye Mtihani ya Taifa wa darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita, ambapo katika matokeo ya kidato cha nne mwaka 2016 ufaulu ulikuwa asilimia 74 mkoa ukiwa nafasi ya 14 kati ya mikoa 26, mwaka  2017 ufaulu asilimia 79.8 nafasi ya 11 na mwaka 2018 ufaulu asilimia 82.5  ukashika nafasi ya 9 kati ya mikoa 26.

Kwa upande wao wanafunzi wa kidato cha nne waliopo kambini  wameshukuru kuwekewa kambi hiyo na wakaeleza imani yao juu ya uwepo wa kambi hiyo ambapo wameomba kambi za kitaaluma Simiyu ziwe endelevu ili ziwasaidie kujifunza na kujiandaa vema na mitihani ya Taifa hatimaye mkoa uweze kufanya vizuri.

"Tunawashukuru viongozi wetu na wazazi wetu kwa kukubali kutuwekea kambi ya kitaaluma, ninashauri kambi hizi zisiishie kwetu ziendelee na kwa wadogo zetu ili mkoa wetu uweze kuongeza ufaulu" alisema Esther Nashoni mwanafunzi shule ya sekondari Bariadi(Bariadi)

Mkuu wa Shule ya Sekondari Simiyu, Mwl.Paul Susu amesema walimu wamejiandaa vema katika kuwafundisha wanafunzi na kuwapa mitihani ya mara kwa mara ili waweze kufanya vizuri, huku akitoa wito kwa wadau mbalimbali wa elimu kujitolea katika ujenzi wa miundombinu ya elimu ili kuwe na miundombinu ya kutosha itakayoongeza nafasi kwa kambi za kitaaluma kufanyika  vizuri.

Kambi ya kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha nne iliyozinduliwa Septemba 05, 2019 ilianza rasmi Septemba Mosi na inatarajiwa kufanyika ndani ya siku 60 kabla ya kufanya Mtihani wa Taifa mwezi Novemba.

MWISHO



Source

Friday, August 30, 2019

MWENDESHA BODABODA ALIYEFARIKI KWA AJALI AZUA GUMZO KUACHA WAJANE 'Wake' 6 NA WATOTO 30

Siri nyingi hufichuka wakati ambapo binadamu anafariki kwani licha ya kuwa ni kinyume na itikadi kumuanika aliyeaga dunia, mambo mengine hasa ya kifamilia huwa vigumu kuyaficha. 


Hayo ndiyo yalifichuka baada ya dereva mmoja wa bodaboda aitwaye Hassan Mafabi (51) mkazi wa Nakatundu Kangulumira nchini Uganda kufariki dunia kwenye ajali ya barabarani pikipiki yake kugongana na gari siku ya Jumamosi wiki iliyopita.

Bodaboda huyo alikuwa na wake 6 na watoto 30 licha ya kazi yake yenye malipo ya wastani hali iliyosababisha watu wengi kushangaa ni vipi aliweza kutekeleza mahitaji ya wake hao wote. 

 Wengi wamepigwa na butwaa baada ya matangazo kuwafikia kuhusu mchango wa kusaidia familia ya marehemu kwani ameacha wajane sita na watoto 30.


Hassan Mafabi mwenye umri wa miaka 51 alikuwa akiishi na wake hao sita na watoto wake na kuchapa kazi kama kawaida huku wengi wasijue kuwa alikuwa na familia kiasi hicho.

 Kulingana na Ugandanz.com, Mafibi aliishi katika kijiji kimoja nchini humo tangu kifo chake barabarani ambapo aligongwa na gari. 


Askofu wa kanisa la Mukono nchini humo alidhibitisha kisa hicho na kuwataka marafiki kujitokeza kuisaidia familia ya Mafibi kwani yeye ndiye alitegemewa kuilisha. 

Wengi hata hivyo walishangaa ni vipi mwendesha bodaboda huyo aliweza kuwalisha wake hao pamoja na watoto 30 ikizingatiwa mapato ya biashara ya bodaboda ni ya wastani tu.

Harmonize Huu ni muda wa kuungana Na Clouds (CMG),Utafika mbali Bro.


Hey Guys...

I Hope mko poa wakubwa,,,Ryt,,??

Okay Fresh

Najua watu wengi nikiwemo Mimi wanajiuliza,Je Ngoma za Harmonize zitaanza kupigwa Clouds baada ya kujitoa kwenye lebo ya hasimu wao?

Hilo swali wengi hatuna majibu.

Nakumbuka kipindi bifu la Diamond na Alikiba linaanza lilikuwa ni bifu kubwa sana Kutokana na ushindani ulio kuwepo,Clouds walijitahid kukuza bifu lile ili angalau kumpunguza nguvu Diamond,kweli kipindi cha mwanzoni lile bifu Nahisi Hata Mond Mwenyewe lilimtetemesha kidogo japo hakutaka kujionyesha wazi,

Hilo bifu liliendelelea ila mwisho wa siku mshindi alikuja kupatikana ambaye kila mmoja anamjua Ni Simba AKA Dangote,Moja ya sababu kubwa za Alikiba kushindwa ni Kutokana na mziki wake kutokuwa na ubunifu,pia utoaji wa nyimbo ukawa ni hafifu kwa madai kuwa nyimbo zake zina ishi so hawez kutoa track kila muda,Hali hiyo ilikuwa tofauti kwa upande wa pila ambaye ni mshindani wake,Diamond Platnumz,yeye aliamini kabisa mziki ni biashara na kama ni biashara lazima ahakikishe walaji wake (Mashabiki) kila baada ya muda flani awape Chakula kipya,Mtindo huo wa Alikiba ilifikia hatua Hata wanao msapoti waachane naye wakiwemo clouds wenyewe wakabaki wanamsapoti kishingo upande,

Mpaka Muda huu Mziki huu wa bongo hauna ushindani tena Bali wamebaki wale wanao mchukia Diamond na kujifanya eti wao ni team mziki mzuri (Team kiba).

Kwa mtazamo wangu hapo juu ni kuwa Harmonize kwa uwezo alionao ni kwamba ana uwezo kwa 70℅ kumtetelesha Diamond endapo akichanga karata zake vizuri,Harmonize anacho takiwa kufanya ni kuwa karibu na clouds na kwa uwezo alio nao wa kuimba na kuachia song back to back naona kabisa Clouds wanamhitaji Konde boy kuliko Alikiba,Alikiba hakuwa chaguo sahihi Bali Jamaa alibebwa na wanao mchukia Diamond ila hawakuwa mashabiki.

Simaanishi Harmonize Anaweza kuwa Sawa na Diamond ila akicheza vizuri Anaweza fika mbali coz Jamaa tayari ana connections na wasanii wengi kwa sasa tofauti na Rich mavoko aliye ondoka akiwa hajajijenga vizuri.

Harmonize Najua kwa Muda huu mfupi atayumba ila akichanga karata zake vizuri Anaweza kuwa mkubwa zaid ya alivyo kuwa WCB,Anacho takiwa kukifanya ni kusimama mwenyewe na kutumia njia zile alizo jifunza kwenye chuo (Lebo yake WCB).

Harmonize Hizo views ulizo kuwa unapata kule You tube hazikuwa zako Bali zilikuwa za Diamond so zisikuteteleshe na kukukatisha tamaa baada ya kuona zimepungua,Huu ni Muda wa kutengeneza views zako ili uone ukubwa wako.

JF
Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...