Monday, June 24, 2019
Maswali muhimu ya kujiuliza kabla ya kuanza kufanya biashara
Watu wengi wanaoingia kwenye biashara huwa wanakuwa na matumaini makubwa sana ya kufanikiwa kupitia biashara hiyo. Matumaini haya huwa yanatokana na kuona wengine wanafanya biashara ile wakiwa wanafanikiwa. Mara nyingine matumaini haya hutokana na kuona kuna watu wanaohitaji kile unachopanga kutoa.
Mara nyingi watu wanapoingia kwenye biashara hujikuta wakiona matumaini yale hayawezekani tena. Hii inatokana na kukutana na uhalisia wa kibiashara tofauti na kile walichokuwa wanafikiria kabla ya kuingia. Na mara nyingi matumaini haya hufa kutokana na soko la biashara kutokuwa la uhakika.
Kama wewe upo kwenye biashara, au una mpango wa kuingia kwenye biashara, hapa kuna maswali muhimu sana ya kujiuliza kuhusu soko la biashara yako. Kumbuka kwamba bila ya mteja wewe huna biashara, hivyo unavyojua zaidi kuhusu wateja wako ndivyo unavyoijua zaidi biashara yako.
Yafutayo ndiyo maswali ya kujiuliza wakati wa kuingia kufanya biashara:
Je biashara ninayotaka kufanya ina wateja?
Hili ni swali ambalo huwezi kuliruka. Ni lazima ujiridhishe kwamba kuna wateja wa biashara yako ili uweze kuendesha biashara husika.
Utajuaje kama kuna wateja wa biashara yako?
Angalia watu wenye shida ambayo biashara yako inaweza kutatua
Angalia mahitaji ya watu ambayo wanayakosa kwenye biashara zilizopo sasa.
Sikiliza malalamiko ya watu kwenye aina ya biashara unayofanya. Kama jibu ni ndio kuna wateja ndio unaweza kuendelea mbele. Kama jibu ni hapana, rudi kwenye meza na boresha wazo lako la biashara.
Je soko lina ukubwa wa kutosha?
Baada ya kujua kwamba kuna wateja wa biashara yako, pia unahitaji kujua kama wateja hawa ni wengi kiasi cha wewe kuweza kuendesha biashara yako vizuri. Unaweza kuwa na wazo zuri sana la biashara na kweli kukawa na wateja ila wateja wenyewe ni wachache kwa wewe kuweza kuendesha biashara yenye faida.
Hakikisha una soko la kukutosha ili uweze kufidia gharama zako za kuendesha biashara na kuweza kupata faida pia.
Je soko linafikika kwa urahisi?
Unaweza kuwa na biashara ambayo ina wateja na wateja ni wengi ila kuwafikia wateja wako ikawa changamoto kubwa sana. Kama wateja wamesambaa sehemu mbalimbali na biashara yako ni ya kuhitaji uwe sehemu moja inaweza kuwa changamoto kubwa kwako. Unahitaji kuwa na biashara ambayo itakuwa rahisi kwako kuwafikia wateja wako ili kuweza kufanya nao biashara.
Angalau kwa kipindi hiki imekuwa rahisi sana kufanya biashara kwa maeneo mbalimbali ila bado kuna maeneo ambayo yana changamoto kubwa.
Usiingie kwenye biashara kabla hujajiuliza maswali hayo matatu. Na kama tayari upo kwenye biashara, jiulize maswali hayo matatu na uone ni jinsi gani unavyoweza kuiboresha biashara yako zaidi ili uweze kuikuza na kupata faida zaidi.
Source
AOMBA MSAADA SERIKALINI BAADA YA KUNYOFOLEWA NYETI ZAKE NA FISI

Jamaa aitwaye Julius Somoire (26) aliyenusurika kifo baada ya kuvamiwa na kuumwa na fisi sehemu zake za siri kaunti ya Kajiado nchini Kenya ameitaka serikali kumfidia kufautia majeraha mabaya aliyoyapata.
Mbali na kumjeruhi sehemu zake za siri, fisi huyo pia alimuuma kwenye mikono na miguuni alipojaribu kuwaokoa mifugo wake aliokuwa akiwachunga eneo la Isinya Jumamosi, Juni 22,2019.
"Fisi huyo aliniuma sehemu zangu za siri, aliniumiza sana na sijui iwapo nitarejelea hali yangu ya kawaida, pia aliniuma kwenye miguu na mikono na kuniacha na majeraha mabaya, " Somoire alisema.
Somoire alikimbizwa katika hospitali ya rufaa ya Kajiado huku wakazi wa Isinya wakifanikiwa kumuua fisi huyo kwa kumpiga kwa rungu na mawe.
Shirika la Wanyama Pori, KWS kwa shambulizi hilo na kulitaka litafute suluhu ya haraka ya kuwazuia wanyama pori kuwavamia wakazi.
Aidha, wakazi hao sasa wanataka Somoire afidiwe wakidai shirika hilo limetepetea kazini na linaweka hatarini maisha ya binadamu.
Chanzo- Tuko
GGM WAKUSANYA BIL 13 KUPITIA KILI CHALLENGE
Washiriki wa Changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro ijulikanayo kwa jina la Kili Challenge 2019 wakishuka wakiwa na Bendera ya Taifa huku wakiimba nyimbo mbalimbali za hamasa mara baada ya kuhitimisha safari ya siku saba ya kupanda mlima huo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Anna Mghwira pamoja na Mkuu wa mkoa wa Geita ,Robert Gabriel wakiwa wamepokea Bendera ya Taifa kutoka kwa washiriki 64 wa changamoto ya kupanda Milima Kilimanjaro ambapowashiriki hao waliipandisha bendera hiyo kileleni.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla ya mapokezi ya washiriki 64 wa tukio la Kili Challenge 2019 akizungumza mara baada ya kuwapokea.
Mkuu wa Mkoa wa Geita ulipo Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) Robert Gabriel akizungumza katika hafla fupi ya kuwapokea washiriki 64 wa changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ukimwi.
Baadhi ya Washiriki.
Makamu wa Rais wa Kampuni ya AngloGold Ashanti wamiliki wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) Simon Shayo akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Baaadhi ya Washiriki wa Changamoto ya Kili Challenge 2019.
Kaimu mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Nchini,(TACAIDS),Jumanne Isango akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghwira akitoa burudani kwa kuimba nyimbo wakati wa mapokezi ya Washiriki 64 wa Changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro ijulikanayo kama Kii Challenge 2019 .
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghira akiwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Geita ,Robert Gabriel ,Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro ,Mhandisi Aisha Amour pamoja na Makamu w Rais wa Kampuni ya AngloGold Ashanti,Simon Shayo wakielekea kutembelea mabanda ya maonesho yaliyokuwepo katika lango la mlima Kilimanjaro la Mweka .
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjao ,Dkt Anna Mghwira akimkabidhi Mkuu wa mko wa Geita ,Robert Gabriel kumbukumbu ya kishika Funguo ( Key Holder) wakati akitembelea moja ya mabanda ya maonesho yaliyokuwa katika lango la Mweka wakati washiriki wa Changamoto ya Kupanda Mlima Kilimanjaro (Kili Challenge 2019 ) wakishuka kutoka kilele cha Uhuru.Nyuma ya Mkuu wa Mkoa wa Geita ni Makamu wa Raisi wa Kampuni ya AngloGold Ashanti wamilki wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita.Simon Shayo.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghwira akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki 64 wa changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro pamoja na kuuzunguka kwa Baiskeli kwa lengo la kuchangisha fedha za Mapambano dhidi ya Ukimwi mara bada ya kuwasili katika lango la Mweka .
Mgeni rasmi katika hafla ya kuwapokea Washiriki 64 wa changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro na kuuzunguka kwa Baiskeli kwa lengo la kuchangisha fedha za Mapambano dhidi ya Ukimwi ,Mkuu wa Mkoawa Kilimanjaro akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine wenzake na wadau .
Na Dixon Busagaga.
.Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira,amewataka wageni kutoka Nje ya nchi, kwa ajili ya shughuli za kijamii, Katika Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, kuepuka kuingilia shughuli za mlima huo.
Mbali na hilo, Mkuu huyo pia aliutaka Uongozi wa Wilaya zinazozunguka Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro na Shirika la hifadhi za Taifa TANAPA, kumaliza migogoro inayohusu eneo la hifadhi hiyo,ikiwemo ya Nusu Mail,ambayo imekuwa ikihusisha wananchi wanaozunguka eneo hilo.
Mghwira ameyasema hayo leo wakati akizungumza kwenye hafla ya kuwapokea wanaharakati 64,waliopanda Mlima kilimanjaro,kwa ajili ya kuchangisha fedha za mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi,Kampeni ambayo imeandaliwa na Mgodi wa madini ya Dhahabu Geita (GGM).
"Ipo migogoro ya Nusu maili,ambayo imekuwa ikizungumzwa kila wakati lakini haiishi,niombe viongozi wa Wilaya na Tanapa,waimalize.Niombe pia wageni kutoka nje ya nchi,ambao wanakuja kwetu,kwa shughuli hasa za kijamii,kujifunza kutoka kwetu,na wasituingilie sana kwenye eneo hili"amesema Mghwira
Aliongeza kuwa"Kila wakati tumekutana na mazingira ya wageni kujiingiza kwenye masuala ya mlima na shughuli zinazofanyika hapa na kutuletea utata mgumu,sababu tunaposhughulika na
Wageni kutoka nje ya nchi,mahusiano yake yanakuwa tofauti kidogo na namna ya kufanya maamuzi"
Mkuu huyo alitumia pia nafasi hiyo, kueleza kuwa,Ukimwi bado ni Tishio mtambuka na umegusa na kuathiri kila nyanja ya maendeleo na kuwataka wadau kushirikiana na serikali,kumaluza tatizo hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Robert Gabriel,alisema katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa ukimwi,watoto wa Kike wameonekana kuwa wahanga wakubwa,na kuitaka jamii na wadau,kushiriki kulinda kundi hilo.
Kaimu mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Nchini,(TACAIDS),Jumanne Isango, amesema kunahitajika ubunifu,ili kuongeza hamasa zaidi,katika kuupanda Mlima Kilimanjaro,kwa ajili ya kuchangisha Fedha za Mapambano dhidi ya Ukimwi.
Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Kampuni ya AngloGold Ashanti kupitia mgodi wa Dhahabu Wa Geita,Simon Shayo alisema zadi ya Bil 13 zimekusanywa katika kampeni hiyo tangu ianze na kuungwa mkono na zaidi ya mashirika yasiyo ya kiserikali 40.
"Tunafurahi kweli na tunashukuru kwa washirika wetu wote na tutaendelea kushirikiana kufanya kila liwezekanalo na kwa ambao pia wangependa kujiunga katika vita hivi hii inamaanisha wakihamsika wapandaji zaidi itasababisha watu binafsi na jamii zaidi kuunga mkono na mpango wa Kili Challenge."alisema Shayo.
Shayo aliwashukuru wafadhili wa changamoto hiyo na wote walishiriki kupanda na kwamba jitihada walizoonesha ni muhimu katika kuchochea tukio hilo wakiwemo waendesha baiskeli ambao waliamua kuweka roho zao juu ili kuhakikisha Tanzania kupitia Kili Challenge inafikia sifuri 3 mwaka 2030.
Poshy Queen afunguka kilichompeleka Bungeni
Siku chache baada ya picha zake kusambaa akionekana na wabunge tofauti kwenye Viwanja vya Bunge jijini Dodoma, huku kukiwa na madai kuwa ameenda kudanga, mrembo anayetikisa na umbo matata katika mitandao ya kijamii, Jacqueline Obeid 'Poshy Queen' amevunja ukimya juu ya safari yake hiyo.
Poshy amesema kuwa anawashangaa sana watu wote wanaomjadili na kumsemea maneno mabaya na kuuliza kuwa yeye kwenda bungeni ni makosa.
"Mbona watu wana matatizo sana, yaani mimi kwenda bungeni ni matatizo jamani au sistahili? Kule kila mtu anakaribishwa kama mgeni wakati mimi kuna jambo lilinipeleka kule na nimejifunza vingi", amesema Poshy.
Poshy ameongeza kuwa asingependa kabisa watu waendelee kumjadili kuhusu yeye kwenda bungeni kwa sababu kila mtu anaruhusiwa kwenda, lakini alivyokwenda yeye ilikuwa kwa sababu maalum ya kipindi cha Bunge la Bajeti ambapo amesomea mambo ya usimamizi wa fedha katika Chuo cha IFM jijini Dar es salaam.
"Kule nilikwenda na mimi kuwasilisha mawazo yangu katika kipindi hiki cha Bunge la Bajeti, licha ya kuhudhuria hata nilivyokutana na baadhi ya wabunge niliwaambia mawazo yangu na wamesema watayafikisha huko", ameongeza Poshy.
Katika habari zilizoenea, Poshy alidaiwa kuwa alikwenda jijini humo kudanga baada ya kupata mualiko na mbunge mmoja ambaye ana uhusiano naye. Poshy ametokea kujizolea umaarufu mitandaoni kutokana na umbo lake matata la namba nane ambalo inasemekana kuwa amelipata ghafla au ni la kutengeneza.
Poshy amesema kuwa anawashangaa sana watu wote wanaomjadili na kumsemea maneno mabaya na kuuliza kuwa yeye kwenda bungeni ni makosa.
"Mbona watu wana matatizo sana, yaani mimi kwenda bungeni ni matatizo jamani au sistahili? Kule kila mtu anakaribishwa kama mgeni wakati mimi kuna jambo lilinipeleka kule na nimejifunza vingi", amesema Poshy.
Poshy ameongeza kuwa asingependa kabisa watu waendelee kumjadili kuhusu yeye kwenda bungeni kwa sababu kila mtu anaruhusiwa kwenda, lakini alivyokwenda yeye ilikuwa kwa sababu maalum ya kipindi cha Bunge la Bajeti ambapo amesomea mambo ya usimamizi wa fedha katika Chuo cha IFM jijini Dar es salaam.
"Kule nilikwenda na mimi kuwasilisha mawazo yangu katika kipindi hiki cha Bunge la Bajeti, licha ya kuhudhuria hata nilivyokutana na baadhi ya wabunge niliwaambia mawazo yangu na wamesema watayafikisha huko", ameongeza Poshy.
Katika habari zilizoenea, Poshy alidaiwa kuwa alikwenda jijini humo kudanga baada ya kupata mualiko na mbunge mmoja ambaye ana uhusiano naye. Poshy ametokea kujizolea umaarufu mitandaoni kutokana na umbo lake matata la namba nane ambalo inasemekana kuwa amelipata ghafla au ni la kutengeneza.
AMUUA KWA KUMKATA SHINGO MCHEPUKO WA MKEWE BAADA YA KUWAFUMANIA WAKIHONDOMOLANA

Maafisa wa polisi eneo la Trans Mara Magharibi kaunti ya Narok nchini Kneya wamemkamata jamaa mwenye umri wa miaka 25 baada ya kupatikana na kosa la kumuua mwenzake aliyekisiwa kuwa mpenzi wa mkewe.
Mathew Langat aliripotiwa kumuua Stanley Bor kwa kumkata shingo baada ya kumfumania akishiriki ngono na mkewe wa miaka 22 nyumbani kwake majira ya saa nne usiku Jumamosi Juni 22.
Kisa hicho cha kushtua kimetokea katka kijiji cha Ng'endale, eneo bunge la Angata Barrikoi kule Trans Mara Magharibi.
Akithibitisha kisa hicho, chifu wa kata ya Angata Barrikoi Paul Kirui alisema mshukiwa alimvamia marehemu kwa mkuki na kumdunga shingoni na kwenye koo.
Mwili wa marehemu ulipelekwa katika mochuari ya hospitali ya Tenwek huku mshukiwa pamoja na mkewe wakitiwa mbaroni.
Chanzo - Tuko
Sunday, June 23, 2019
Tumia matunda haya ili kuboresha Ngozi yako
Wakati mwingine ili uweze kuboresha mwonekanao wa ngozi yako si lazima utumie makemikali yenye viambatano vyenye sumu ili uweze kufanya hivyo, bali inahitajika uweze kutumia matunda ambayo yana msada mkuubwa wa kuweza kufanya ngozi yako ing`are.
1. Parachichi.
Tunda hili limekuwa maarufu sana kwa kutengenezewa juisi lakini huenda watu hawalipendi kwa sababu kwa kutokuwa na sukari katika radha yake. Tunda hili lina vitamin kibao, ambapo pia huongeza mafuta mwilini kwa wale walitumialo mara kwa mara, wanashauriwa kula au kunywa juisi ya parachichi wakati wowote endapo kama huna matatazo yeyote yananahusiana na kuzidi kwa mafauta mwilini. Pia tunda hili huongeza uzito endapo utalitumia mara kwa mara.
2. Apple.
Hili ni tunda maarufu sana duniani lihusishwalo na wapendanao, lakini tunda hili pamoja na kupema umaarufu mkubwa duniani na kuwa na vitamin na madini kibao, pia lina kazi sana katika kukupa muonekano mzuri wa ngoz ya mwili wako. Tunda hili husaidia kuboresha mzunguko wa damu pamoja na kuhifadhi ngozi isipoteze uhalisia wake.
3. Ndizi.
Hili pia ni tunda lenye jina kubwa kwa watu wengi wanaojali ulaji wa wa matunda, kwani ni tamu na lenya radha safi. Tunda hili husaidia kulainisha ngozi ya uso iliyokauka, kwa mfano utakuta kuna baadhi ya mafuta au rosheni zimechorwa ndizi. Kula ndizi ili urekebishe ngozi ya uso wako pamoja na kuupa uwezo mzuri wa umeng`enyaji chakula.
4. Papai.
Ni tunda sahihi kabisa kati kukupa ngozi yenye mafauta, kurudishia au kuziba majeraha ya mwili. Papai pia hung`arisha ngozi rangi ya ngozi yako, yote haya hufanyika enzyme inayotokana na papai ambayo huitwa papain. Enadapo kama utaka kutumia papai katika ngozi yako, basi chukua asali changanya na papai liloiva nap aka usoni kwako kwa dakika kumi kisha safisha kisha utona kitakachotokea katika uso wako, utaonekana na kama ngozi ya mtoto wa siku moja.
Asante na endelea kutembelea Muungwana blog kila wakati.
Source
APL YA KIGOMBE MABINGWA WA LIGI YA AWESO CUP PANGANI
Kaimu Mkuu wa wilaya ya Pangani Godwin Gondwe kushoto akimkabidhi Kombe Nahodha wa timu ya APL ya Kigombe ambao ni Mabingwa wa Ligi ya wilaya ya Pangani Maarufu kama Aweso Cup kulia anayeshuhudia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani Jumaa Aweso (CCM) Ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji .
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kulia akiwa ameshika kitita cha shilingi milioni moja kwa ajili ya kumkabidhi mshindi wa mashindano hayo kushoto ni Kaimu Mkuu wa wilaya ya Pangani Godwin Gondwe ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Handeni
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akizungumza kwenye fainali ya Ligi ya Aweso Cup
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani Seif akizungumza wakati wa fainali hizo.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akiwa amebebwa na baadhi ya wapenzi na mashabiki wa soka wilayani Pangani mara baada ya kumalizika Ligi ya Aweso Cup
Katibu wa Kamati ya Mipango na fedha wa Klabu ya Coastal Union Salim Bawaziri kushoto akizungumza wa kwanza kulia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) wa pili kutoka kushoto akiwa kwenye jukwaa kuu na Kaimu Mkuu wa wilaya ya Pangani Godwin Gondwe ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Handeni kulia ni Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gipson George wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye Ligi hiyo
Kikosi cha timu ya Wa2020 wakiwa kwenye Picha ya Pamoja
Kikosi cha timu ya APL ya Kigombe
Sehemu ya wananchi waliojitokeza kuhudhuria fainali hiyo
Sehemu ya mashabiki wa soka wilayani Pangani wakifuatilia mashindano hayo
Wapenzi na mashabiki wa timu ya APL ya Kigombe wakishangia ushindi huo
Sehemu ya wananchi wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye Ligi hiyo
TIMU ya APL FC ya Kigombe wilayani Muheza mkoani Tanga imetawazwa mabingwa wapya wa Ligi ya wilaya ya Pangani maarufu kama Aweso Cup baada ya kuifunga Wa 2020 FC mabao 2-0 kwenye mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa soka Kumba.
Kutokana na Ubingwa huo APL Kigombe walifanikiwa kukabidhiwa Kombe la Mashindano hayo, Kitita cha Sh.Milioni moja na Ngom'be huku mshindi wa pili wa 2020 FC akipata kitita cha sh.laki sita na elfu sabini ya mbuzi na medali za dhahabu.
Mshindi wa pili kwenye Mashindano hayo timu ya Wa 2020 FC walikabidhiwa medali, kitita cha laki sita, mbuzi na medali ya dhahabu kwa wachezaji wake huku mshindi wa tatu naye akipata kitita cha sh.laki nne na mbuzi.
Mashindano hayo yamedhaminiwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji huchezwa kila mwaka yakiwa na lengo la kuibua na kukuza viwango vya soka mkoani humo ambayo yalishirikisha timu 16.
Mchezo huo wa fainali ya Ligi hiyo ulichezwa kwenye viwanja vya Kumba mjini Pangani uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wasanii wa bongo movie.
Katika mchezo huo mabao ya APL ya Kigombe ambao ndio mabingwa wapya yalifungwa na Malimo Magembe kwenye dakika ya 35 baada ya kutumia uzembe wa mabeki wa timu pinzani kupachika wavuni bao hilo.
Baada ya kuingia bao hiloWa 2020 FC waliweza kurudi kujipan ga na kuanza kufanya mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa APL ya Kigombe bila mafanikio kutokana na mashuti waliokuwa wakijipa wachezaji wao kugonga mwamba na kutoka nje.
Shambulio hilo liliweza kuwaamsha APL Kigombe ambao baada waliweza kurudi kujipanga na kupelekea mashambulizi langoni
Akizungumza kabla ya kukabidhi zawadi kwa washindi Naibu Waziri Aweso alisema kwamba Ligi hiyo imekuwa na mafanikio makubwa kwani imewezesha kupandisha timu nne kwenye Ligi ya mkoa na baadae anaamini zitafika Ligi Daraja la kwanza na hatimaye Ligi kuu
Alisema kupitia michezo wilaya ya Pangani inaweza kutoa wachezaji nguli kwenye soko kama vile Mbwana Samata na Thomas Ulimwengi ambao wanaweza kuitangaza nchi kupitia soka
Aidha aliwataka kuendelea kushikamana na kupendana huku akikitaka Chama cha mpira wilayani Pangani kianzishe mashindanbo kwa upande wa wanawake ikiwemo rede na mpira wa miguu atadhamini.
Kwa upande wake Katibu wa Kamati ya Mipango na fedha wa Klabu ya Coastal Union Salim Bawaziri alisema kwamba kupitia mashindano ya Aweso Cup wameona vipaji vya wachezaji huku akieleza watachukua wachezaji 10 ambao watawatumia kwenye Ligi kuu.
Waziri Lugola azidi kukomalia suala la Polisi na Bodaboda
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Magufuli kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi iliyodhamiria kupambana na umaskini na changamoto ya ajira, Serikali ipo makini na wanahakikisha wananchi wanapambana na umaskini na tatizo la ajira.
Amesema hayo alipofanya ziara ya kushtukiza katika Kituo cha Polisi Gogoni kilichopo Wilaya ya Kipolisi Kimara, Wilayani Ubungo, jijini Dar es Salaam, leo kwa lengo la kuangalia utendaji wa Polisi kituoni hapo.
Aidha, amesema vijana wengi wameamua kupambana na umaskini kwa kujiajili kupitia pikipiki maarufu bodaboda lakini kumekuwa na malalamiko mengi ambayo yalifika hadi bungeni kwa vijana hao kuonewa, kupigwa na kunyang'anywa pikipiki zao.
"Nilitoa maagizo kwa Jeshi la Polisi juu ya bodaboda ambazo zinaweza kukamatwa na kuwekwa katika vituo vya polisi; bodaboda zinazostahili kukamatwa ni zile zilizohusika na uharifu, zilizohusika na ajali, zilizopotea na kuonekana na zile zilizookotwa," alisema Lugola.
Aliongeza kuwa, bodaboda nyingine zinazokamatwa na makosa mengine ya usalama barabarani kwa kupakia abiria zaidi ya mmoja maarufu kama mshikaki na kutovaa kofia ngumu na mshtakiwa anaweza kutozwa faini ambayo italipwa ndani ya siku saba.
Hata hivyo, Waziri Lugola baada ya ziara yake hiyo ambapo alizikagua bodaboda mbalimbali kituoni hapo, alisema amejiridhisha kwa kukuta bodaboda zote zipo kwenye makundi aliyoyaainisha na amelipongeza na amempongeza Mkuu wa Jeshi hilo, Simon Sirro kwa maelekezo yake aliyoyatoa kwa Jeshi hilo kufanyiwa kazi.
MREMBO Lulu Michael AMKA Katika Usingizi, Aamua Kufungua Duka la nguo
Muigizaji maarufu bongo , ambaye pia linapokuja suala la fashion huwa hakosei, kupitia ukurasa wake wa instagram , ametangaza ujio wa collection yake mpya ambayo ameipa jina la EM collection , ambapo ametangaza kuzindua duka lake jipya la nguo hivi karibuni,
Lulu Michael toka ametoka jela amekuwa katika mahusiano na CEO wa EFM Majizo
Subscribe to:
Posts (Atom)
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...


















