Thursday, September 20, 2018

Mambo Wanawake Wanayotaka Katika Mapenzi Lakini Hawezi Kusema


Mara nyingi wanawake wamekuwa watu wa kukaa kimya bila kusema wanataka nini ili kuridhishwa katika mapenzi na mbaya zaidi katika swala zima la mahaba, sasa basi kama wmwanaume inabidi kujua nini mwanamke wake anataka kabla ya tendo husika.

Mwanamke anapenda ufate anachotaka.

Katika mapenzi wanawake wanapenda ufanye kile wanachokitaka japo ni vigumu kujua mwanamke anapenda nini. Kwa hiyo kama ni vigumu kujua kitu gani anapenda basi ni vizuri kuwa makini na kugundua ni kitu gani hapendi ili usimfanyie ambacho hapendi na ufanye anachopenda. Japokuwa si wanawake wote wanaweza kukwambia ni nini hasa kinawauzi, kuogopa kukuudhi, hivyo inawafanya wapate shida sana na kuweka maisha yao yawe magumu. Kwa sababu hiyo wewe kama mwanaume unapaswa kuwa makini na matendo yao ili kujua tofauti ya vitu ambavyo hawapendi na vile vinavyowapa furaha. Kisha fanya vile wanavyovipenda.

Hupendela tendo la ndoa lidumu muda mrefu.

Wanawake hupenda tendo la ndoa lidumu walau kwa dakika mbili. Na wanatamani ikiwezekana hata ikibidi ifanyike siku nzima. Sio muda tuu ndio muhimu bali hata kile unachofanya. Wanaume wengi kujali kujizuia, ilimradi wakae muda mrefu katika tendo, lakini kutokana na tafiti hili sio sababu, wanawake wengi hupenda zaidi ya muda mrefu, hupenda kuungana na wewe kihisia kupitia kushikana, kubusu nakadhalika. Wakati wanaume wengi huwa hawafanyi na kukazania tu kukaa muda mrefu kujua kuwa ndio wanawake wanachotaka. Kwa hiyo wanapenda tendo la ndoa lidumu lakini lisichoshe.

Usitumie nguvu katika mapenzi.

Wanawake wanataka wanaume walio jasiri wa kufanya nasio wanaotumia nguvu na ubabe. Wanaume wengi huwa hawajui tofauti ya ujasiri na kutumia nguvu, hivyo wasikiapo kuwa inabidi uwe na ujasiri wanadhani kuwa kuna kutumia nguvu na mwisho kuwaumiza wapenzi wao, wanawake wengi wamekuwa wakikerwa na kuogopeshwa na mambo ambayo hufanyiwa na wanaume zao, kipindi ambacho wanaume wakufikiri kufanya hivyo ni kuwa na ujasiri. Wanawake hutamani sana wanaume wangejirekebisha na kujua maana halisi ya kuwa na ujasiri kwamba sio kutumia nguvu na ubabe.

wanawake wengi hawafanani.

Wanawake wanapenda wanaume wajue kuwa sio wanawake wote hupenda vitu sawa. Wanaume wengine hufikiri kuwa kwa sababu mpenzi wake wa zamani alikua anapenda kufanyiwa alikuwa basi na huyu wa sasa atakuwa hivyo hivyo, hii inatokea kuwachanganya sana wanawake, na kukereka kwa baadhi ya mambo, huku mwanamke akiwa hana jinsi bali kuvumilia tu, na mwisho wa siku ndio unakuta, ananza kutafuta njia ya kukukwepa. Kwa hiyo mwanamme anatakiwa amjue mpenzi wake kibinafsi yeye kama yeye na sio kumjua kwa kumfananisha na wanawake wengine. Mwanamme amfanyie mpenzi wake kama anavyopendelea na sio kama anavyofikiri wanawake wanapendelea.

Kuna faida kubwa wa faragha na makosa ya mwanamke


TENDO la ndoa lina umuhimu wake. Kwa namna moja au nyingine linakamilisha maana nzima ya mapenzi. Ni kama vile kachumbari kwenye pilau. Si kwamba pilau haliliki bila kachumbari lakini ikiwepo, utamu unakamilika. Ili kuleta ustawi wa penzi, mwanamke ana wajibu wa kutenda tendo hilo kikamilifu, hali kadhalika mwanaume. Mmoja kati yao anapolifanya chini ya kiwango, humuweka mwenzake njia panda. Aone kuna kitu hakijakamilika.

Hakijakamilika kwa sababu amemuacha njiani. Mwenzake alikuwa anahitaji kuendelea na safari, lakini yeye ameikatisha. Ni sawa na mtu kuwa na kiu ya maji halafu, ukapewa maji kiduchu. Kiu inabaki palepale, unatamani kupata maji mengi ili uikomeshe lakini mwenzako hana habari.

Kwa kuwa uhusiano unajengwa na vitu vingi likiwemo hilo, linapokuwa linafanyika chini ya kiwango, uhusiano unakuwa haujakamilika. Upungufu utaonekana na taratibu penzi linaweza kuyumba. Kachumbari ikikosekana kwenye pilau, ladha itatoka wapi?

Nirudi kwenye msingi wa hoja sasa. Kwa kuzingatia kwamba unyumba ni kiunganishi adimu kwenye uhusiano, baadhi ya wapendanao hususan wanawake hupenda kutumia nafasi hiyo kuwanyanyasa wenzi wao. Wanaugeuza unyumba kuwa fimbo ya kuwachapia wenzi wao.

Mwanamke anaona ili kumkomoa mwanaume kutokana na kosa fulani, anamnyima unyumba. Anaamini ni silaha kubwa. Kwamba mwanaume aliyekamilika, lijali kabisa, hata iweje lazima atakuwa na hitaji hilo la mwili. Atahangaika huku na kule akiwa faragha ili mradi tu akate kiu yake. Nimesema wanawake wengi hupenda kuitumia silaha hiyo maana kwa sababu kimaumbile, wao ni rahisi sana kujizuia kuliko wanaume.

Wanaamini wanaume si wavumilivu. Watahangaika, mwisho wa siku watahitaji tu 'huruma' ya wanawake. Penzi wanaligeuza kama hisani. Yeye ndiye mmiliki wa tendo hilo. Anataka atafanya, asipotaka basi hakuna kitakachoeleweka. Wanaamini kwamba ili mwanaume apewe, inabidi awe mpole. Ajishushe. Kama alikosea, anapaswa kuomba kwanza msamaha, asamehewe ndipo mambo yaendelee. Vinginevyo ataishia kulala mzungu wa nne.

Itakuwa siku, wiki, mwezi na hata miezi kadhaa. Hadi kieleweke. Mwanaume akubali kujishusha, apewe unyumba. Asipofanya hivyo kazi anayo. Aandike maumivu endelevu mpaka pale atakapoamua kujishusha na kutambua thamani ya mwenzi wake.

NI KOSA KUBWA
Si busara kutumia unyumba kama silaha ya kumchapia mwenzako pale anapokosea. Ni bora ukamuadhibu kwa mambo mengine lakini si unyumba. Kile ni kiunganishi muhimu, kinapokosekana, madhara yake ni makubwa. Usaliti huanzia hapo. Kumnyima mwenzi wako unyumba, ni kukaribisha mwanya wa usaliti. Atavumilia, naye ni binadamu anaweza kuchoka. Anaweza kutafuta jinsi ya kufanya. Akiifanya, akinogewa unafikiri nini kitatokea? Hataona umuhimu wako.

Atakulinganisha wewe na yule aliyechepuka naye. Ataona amepata tiba sahihi. Ni rahisi kukufanya wewe ni mlezi wa familia. Mwanamke naye akigundua, naye anaweza kuona njia nzuri ya kumkabili ni kujibu mapigo. Hapo ndio kunakuwa hakuna mapenzi. Kama ni ndoa itakuwa rehani. Muda wowote inaweza kuvunjika, kila mmoja akachukua njia yake.

UNYUMBA SI PROMOSHENI
Chondechonde, usimpe mwenzi wako unyumba kama vile unamzawadia. Mpe kama ni wajibu wako. Ona kabisa una kila sababu ya kumpa maana wewe ndiye kimbilio lake. Wewe ndiye unayepaswa kumtimizia mahitaji yake ya kimwili, kiakili na hata kifikra.

Kama amekosea, kasirika, nuna, baadaye hasira zikiisha, mueleze pale alipokukwaza. Kama binadamu, atajipima na ataelewa makosa aliyoyafanya. Hata kama mna ugomvi, linapokuja suala la unyumba hupaswi kulifanyia mzaha maana ni hatari kwa mustakabali wa penzi lenu.

TENDO NI MUHIMU KWELIKWELI
Kwanza ndivyo tafsiri rahisi ya vitabu vya dini. Vinasema, enendeni mkaijaze dunia. Hamuwezi kuijaza dunia pasipo kufanya tendo hilo. Utofauti wake tu, kuna wanaolifanya kihalali kwa maana ya kufunga ndoa kwanza lakini kuna wengine wanaanza kushiriki kabla hata hawajafunga ndoa!

Wednesday, September 19, 2018

Wolper amlilia Soudy Brown na Maua Sama, ajitosa kuwaombea msamaha ‘jamani ndani sio kuzuri’

Muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Jacquiline Wolper amejikuta akiumia kwa tukio la kukamatwa kwa mtangazaji wa kipindi cha SHILAWADU Soudy Brown na Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Soudy Brown. Wolper kupitia ukurasa wake wa Instagram, amesema anaomba viongozi wakubwa wa nchi wawaachie wasanii hao kwani walikuwa kwenye utafutaji na badala yake adhabu waliyoipata kwa …

The post Wolper amlilia Soudy Brown na Maua Sama, ajitosa kuwaombea msamaha ‘jamani ndani sio kuzuri’ appeared first on Bongo5.com.


Source

Mambo muhimu ya kuzingatia kilimo cha bustani


Kilimo cha bustani kinahusika na uzalishaji wa mazao ya aina ya mboga, matunda, viungo na mimea ya mapambo.

Kilimo cha bustani ni chanzo cha ajira na pato kwa wakulima na watu wengine. Mboga na matunda vinatupatia virutubisho vya kujenga, kutia nguvu na kulinda mwili.

Zaidi ya hivyo, mimea ya mapambo hutumika katika kuremba na kuboresha sehemu za makazi, majengo, barabara na sehemu nyingine za wazi za jumuia.

Hata hivyo, unapowaangalia wakulima wengi mazao ya bustani hasa yale ya mbogamboga, utagundua wengi wamejikita katika uzalishaji wa mazao hayo, kwa lengo la kukidhi mahitaji ya familia pekee.

Hawa ni wakulima wasio na wigo mpana wa kuzalisha kwa kulenga soko kubwa na kupata kipato cha kudumu, japo mazao hayo yana sifa ya kuwa na soko zuri.

Ni muhimu kuhakikisha kunakuwapo mifumo mizuri kuanzia kwenye uzalishaji, uhifadhi, usindikaji na upatikanaji wa taarifa sahihi za masoko.

Haya yakifanyika, kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuwawezesha wakulima kuuza mazao yao kwa faida kubwa na kuwawezesha kukua kiuchumi.

Mambo muhimu ya kuzingatia katika uzalishaji

Hata hivyo, ili kuzalisha kwa kiwango kikubwa, mkulima wa mazao ya bustani anapaswa kuzingatia baadhi ya mambo muhimu ikiwamo kuwa na taarifa sahihi na za kutosha kuhusu zao analolima.

Mkulima anatakiwa kuwa na taarifa zote muhimu zinazohusiana na zao analotegemea kushughulika nalo.

Taarifa hizi zinajumuisha upatikanaji wa mbegu bora, hali ya hewa inayopendekezwa kwa zao husika.

Mengine ni taarifa kuhusu magonjwa na wadudu wanaoweza kulishambulia zao hilo na namna ya kuyakabili, pamoja na uhitaji wake katika soko la ndani na la nje.

2.Misingi ya uzalishaji: Ili mkulima aweze kuzalisha kwa tija na kwa gharama nafuu wakati huo

huo akilinda afya yake na ya walaji, ni muhimu kuzalisha kwa misingi ya kilimo hai.

Fanya uzalishaji wa mazao kwa kuzingatia misingi hii kuanzia kwenye mbegu kwa kutumia mbegu zilizozalishwa kwa misingi ya kilimo hai, matumizi ya mbolea hai, dawa za kudhibiti magonjwa na wadudu pamoja na uhifadhi wa mavuno au mazao yako ghalani au katika usindikaji.

Kilimo hai ni aina ya kilimo kisichotumia madawa wale kemikali za viwandani. Bidhaa zitokanazo na kilimo hai zinaelezwa kuwa na ubora maradufu kuliko bidhaa zitokanazo na madawa na mbolea za viwandani.

3.Eneo na hali ya hewa:

Kabla mkulima hajafikiria juu ya kulima zao fulani, ni lazima ahakikishe kuwa ana eneo la kutosha kwa ajili ya mazao yake

Lakini pia ahakikishe kuwa hali ya hewa ya eneo hilo inaoana na zao analotaka kulima.

4.Gharama za uzalishaji:

Jambo hili ni la msingi kwani huwezi kufanya kilimo bila kuingia katika gharama za uzalishaji.

Gharama hizi ni pamoja na ununuzi wa mbegu, maandalizi ya shamba, utunzaji wa zao shambani kwa kudhibiti wadudu na magonjwa, uvunaji na upelekaji sokoni au usindikaji.

5.Upatikanaji wa soko

Suala la soko ni la msingi na ni la wakati wote, kuanzia kipindi cha utafutaji taarifa ya zao husika, wakati zao likiwa katika hatua ya awali ya uzalishaji na hata linapokuwa tayari kwenda sokoni.

Ni muhimu kwa mkulima kutafuta soko la mazao yake ili aweze kuuza kwa bei iliyopo sokoni na ikiwa bei

imeshuka kwa ghalfa bila kutarajiwa, aweze kufikiri namna nyingine ya kutatua tatizo hilo hasa kwa kutumia njia mbadala kama vile kufanya usindikaji wa zao lake.

6.Mikataba ya ununuzi:

Mbali na upatikanaji wa taarifa za masoko kwa wakulima wa bustani, ni muhimu pia wakulima kuhakikisha kunakuwapo mikataba inayoeleweka baina yao na wanunuzi.

Mikataba hii itawawezesha kujua wanazalisha nini, watapata huduma wapi, watauza wapi, watauza kwa nani na watauza kwa bei gani.

Aidha, kabla wakulima hawajaingia katika kufanya mikataba, ni muhimu wakawa na uelewa mkubwa wa namna ya uuzaji wa mazao hayo ya bustani ndani ya nchi na hata nje ya nchi, bila kudanganywa na bila kudidimizwa ili kuendeleza uchumi wao wenyewe na wa nchi kwa jumla.

7: Kulima kulingana na uhitaji

Hili linawagusa wakulima wengi hasa wanaolima kwa kufuata mkumbo kama ilivyozoeleka hivi sasa katika jamii zetu.

Ni kweli hamasa za kutaka watu wajiingize kwenye kilimo ni nyingi, kubwa na zina umuhimu, lakini wakulima hawana budi kutafakari kabla ya kuamua kuingia kwenye kilimo fulani.

Lazima wakulima wahakikishe wanalima kulingana na uhitaji wa walaji na si kulima kwa mazoea au kwa vile kila mmoja analima.

Kwa mfano, sio busara kutaka kulima matikiti kwa kuwa ndilo zao linalolimwa na kila mtu eneo uliopo. Tatuta zao ambalo mahitaji yake ni makubwa, kwa kuwa unakuwa na uhakika wa soko lake

Over 100 leaders attend capacity-building training by party registrar

Over 100 political party leaders have today, September 19, responded to the Registrar of Political Parties' call to attend a two-day workshop that seeks to impart knowledge on the importance of political party institutionalization in the country.
Source

Nora wa Bongo Movies Aamua Kujivua..."Kazi Niliyotumwa na Mungu Nimeimaliza"


Msanii wa filamu nchini, Nuru Nassoro maarufu kama Nora ametangaza rasmi kuachana na masuala ya sanaa ya uigizaji, huku akidai hata ikitokea amefariki hii leo atajisikia furaha kwa kuwa kazi iliyomleta duniani ameikamilisha.

Nora ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Instagram huku akiwakosoa baadhi ya wasanii wa sasa wa filamu kuwa wamejawa na utandawazi, jambo ambalo linawapelekea kufanya mambo yasiyokuwa na maadili kwenye mitandao ili kusudi wapate kusifiwa, kujulikana na kupendwa.

"Nimeacha historia kwenye maisha yenu, kila mnapo nikumbuka kumbukumbu nzuri za furaha zinawajia kwenye vichwa vyenu, mpaka mnatamani enzi hizo zingekua zinarudi. Namshukuru MUNGU wangu sana kwa hili kwani ni kitu kizuri ukifanya kitu na watu wakakukumbuka kwa mazuri kiukweli ninapata furaha mnoo, ambayo haielezeki...

Japo najikuta najisikia vibaya wengine wanaposema walikua wanafukuzwa kwenye 'sitting room' za watu lakini ilibidi wakae madirishani na ikibidi wakate madirisha ya watu, wengine walikua wanakalishwa chini au inawabidi wafanye kazi ili jioni inapofika waangalie kipindi. Ninawatangazia rasmi nimeacha kuigiza.", ameandika Nora.

Pamoja na hayo, Nora ameendelea kwa kusema kuwa "mapenzi yenu yalikuwa sio ya kawaida wallah, hata nikifa leo kazi ilio nileta duniani ya kuwa burudisha na kuwafundisha nilifanya kwa ufasaha. Ama kweli enzi haziwezi kurudi, sasa hivi dunia imekua ya utandawazi watu wamekuwa wakilazimisha kupendwa, kusifiwa, kujulikana, inafikia wakati maadili hamna, mazoea ya kukaa pamoja kama familia na kuburudika na kujifunza".

Mbali na hilo, Nora amesema kuwa anajivunia kuwa msanii wa zama za zamani kuliko sasa, kwa kile alichokidai kwamba kizazi hiki kimeharibiwa na utandawazi katika kila kona.

"Nimeacha alama ambayo haitofutika daima niko hai au nimekufa, alama ambayo hata kwa Mungu ninacho cha kujitetea na akanielewa kwa kuwa siku lazimisha umaarufu ulikuja wenyewe, sikudanganyika na dunia bali niliishi kadri umri ulivyo nihitaji. Mara zote niliipigania heshima yangu kwenye kila kitu kama binadamu nilikosea lakini sio kwa makusudi eti ili niitawale dunia", amesisitiza Nora.

Nora alianza kujipatia umaarufu kwa jamii kupitia 'Kaole Sanaa Group', ambao walikuwa wanafanya maigizo yaliyokuwa yanayoeneshwa katika televisheni ya ITV.

Nora ni miongoni mwa wasanii waliowahi kuigiza na marehemu Steven Kanumba katika filamu ya 'Dangerous Desire' ambayo alivaa uhusika wa mke wa Kanumba.

Hotspots, not trouble spots: Africa seeks tourism boom

Africa draws just five percent of the world's tourists despite boasting attractions ranging from the Pyramids and Victoria Falls to wildlife safaris and endless strips of pristine beach.
Source

NISSAN SAFARI BXB INAUZWA

 Nissan safari (BXB)
Year:1990
Cc:4169
Km: 140,700
Fuel: diesel
Engine: TD4
Forg lights
Gari imetunzwa vizuri,mmiliki anaweza kubadilishana na gari nyingine
Price: 7:5m
Call: 0713-903250
          0784-331821









Source

MASANJA MKANDAMIZAJI KAACHIA WIMBO MPYA UNAITWA KEMEA PEPO... HUU HAPA

Masanja Mkandamizaji anakukaribisha kusikiliza wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Kemea Pepo. Usikilize hapa.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...