Wednesday, June 18, 2025
Bilioni 1.4 zatekeleza Miradi ya Maendeleo Kata ya Ufana 2020-2025.
Thursday, June 5, 2025
TBS YASISITIZA UMUHIMU WA VIWANGO KATIKA MAONESHO YA BIASHARA TANGA
Akizungumza katika maonesho hayo, Afisa Udhibiti Ubora wa TBS, Bw. Abdul Ngozoma, ametoa wito kwa wajasiriamali kujitokeza kwa wingi kuthibitisha ubora wa bidhaa zao kupitia Shirika hilo.
BASHUNGWA AHIMIZA WAANDISHI WA HABARI KUHAMASISHA AMANI NA USALAMA
Source
Madaktari bingwa wamtibu mzee aliyekuwa na tatizo la kuoza sehemu ya utumbo.
KINGBET YAZINDUA KAMPENI YAKE YA "CHA KUKALIA" KUWASAIDIA WANAOCHEZA AVIATOR
MWENGE WA UHURU KUZINDUA, KUWEKA MAWE YA MSINGI MIRADI 13 YA RUWASA YENYE THAMANI YA BILIONI 16.713

Na Hadija Bagasha- Tanga
JUMLA ya Miradi 13 katika Sekta ya Maji yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 16.713 inatarajiwa kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 Mkoani Tanga na itakayohudumia wananchi zaidi ya 85,017 hatua inayotajwa kuwapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu ili kufuata huduma hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Juni 5 mwaka huu, Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Omari Lugongo alisema kwamba miradi hiyo itanufaisha wananchi 85,017 ambao wanapata huduma ya maji safi na salama na kuondokana na adha ambazo walikuwa wanazipata awali.
Alisema kila Halmashauri itakuwa na mradi na miradi 6 ya uzinduzi,miradi 5 ya uwekeji mawe ya msingi katika miradi hiyo itakayozinduliwa itajumuisha vijiji 12 lakini kuwahudumia watu 28000 na karibia asilimia 1 ya wakazi wa mkoa wa Tanga.
Alisema kwamba pia kuna miradi ya uzinduzi katika Jiji la Tanga kupitia Tanga Uwasa ambapo kutazinduliwa mita za malipo kabla na ni maelekezo ya Rais Dkt Samia Suluhu ya viongozi wa chama na serikali ili kuhakikisha maji yanatumika kwenye viwango lakini yanatumika wananchi waweze kulipia kulingana na uwezo wao.
Aidha alisema kutakuwa na uzinduzi kwenye Jiji la Tanga ya Mita za malipo kabla 4,000 zitazinduliwa na mwenge pamoja na kuwepo na miradi mengine ya uzinduzi kwenye wilaya za Handeni ,Lushoto ,Mkinga na mwengine utakuwa ni mradi wa uwekaji mawe ya msingi.
Alisema katika wilaya ya Pangani kwenye Jimbo la Waziri wa Maji kutakuwa na mradi wa uwekeji jiwe la msingi mradi wa maji Mkwaja ili uweze kukamilika kwa kipindi kifupi kijacho na katika miradi wanayoweka uzinduzi ni Kwedizinga wilaya ya Handeni Vijiji,Mgombezi Korogwe Mjini na hapo wamejenga visima 900 vya Rais Samia Suluhu.
Aidha alisema kati ya visima hivyo ambavyo ni mradi maalumu wa kutatua changamoto ya maji kwenye maeneo yasiyokuwa na maji wilaya ya Korogwe watakuwa na mradi wa uzinduzi na wilaya ya Muheza watakuwa na mradi wa visima 900 watakwenda kuweka jiwe la msingi lakni watu wameshaanza kupata huduma ya maji ikiwemo wilaya ya Mkinga wanazindua mradi wa maji Gombero na wilaya ya Tanga ambazo ni Mita za Luku za Maji na wilaya ya Lushoto ni mradi wa Funta –Wanga
Meneja huyo alisema pia kuna mirdi mitano ya uwekaji wa mawe ya msingi kwenye eneo la Kwamaligwa wilaya ya Kilindi ambao utahudumia vijiji saba na mradi wa Maji kwamahizi ambao utahudumia eneo la Handeni Mjini.
Alieleza pia Mwenge huo utatembelea mradi wa ukarabati miundombinu ya maji Lushoto Mjini ambao utaboresha huduma kwa wakazi zaidi 23,000 na uwekeji jiwe la msingi mradi wa maji Mkwaja na Visima 900 wa Rais kwa wilaya ya Muheza ambapo miradi hiyo yote inakwenda kuwahudumia wakazi wa Tanga asilimia 3 hivyo wanategemea miradi hiyo itakapokamilika itasaidia kuboresha asilimia 3.3 ya wakazi wa Tanga wakati ile asilimia 1 ya miradi itakayozindua nayo inakuwa imeshakamilika.
"Nimpongeze Rais Dkt Samia Suluhu kwa utekelezaji wa miradi hii pamoja na Mkuu wa Mkoa kwa kuendelea kutuongoza vema katika mkoa wetu pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa huu Rajab Abdurhaman" alisema
Mwenge wa uhuru unatarajiwa kuwasili Mkoani Tanga Juni 6 mwaka huu na kukimbizwa katika maeneo mbalimbali kwenye Mkoa huo.
WAZEE WAMSHUKURU RAIS SAMIA KUBORESHA HUDUMA KWA USTAWI WAO

MBELLAS HEAVENLY CAKES - KARIBU FURAHIE KEKI BORA KWA BEI RAFIKI

🌟 MBELLAS HEAVENLY CAKES 🌟
Classic Cakes for All Occasions 🎂✨
Unatafuta keki nzuri, tamu na ya kipekee kwa tukio lako?
Mbellas Heavenly Cakes ndio jibu lako! Tunatengeneza keki za kiwango cha juu kwa matukio yote:
🎉 Siku za Kuzaliwa
💍 Harusi
💝 Zawadi za Wapendanao
🎄 Sikukuu na Sherehe
👶 Baby Shower & Welcome Home
🎓 Graduation na zaidi!
🍰 Keki zetu ni:
✔️ Zenye ladha ya kipekee
✔️ Muonekano wa kuvutia
✔️ Ubunifu wa kisasa
✔️ Zinapatikana dukani kwetu na kwa oda maalum kulingana na tukio lako
📍 Tunapatikana Kahama Mjini Kahama - Shinyanga
📞 Wasiliana nasi leo:
📲 0753 998 330
📲 0654 717 970
📸 Instagram: @mbellas_hevenly_cakes
🔖 Karibu sasa ufurahie keki bora kwa bei rafiki!
📅 Tunapokea oda kila siku — book mapema!
Wednesday, June 4, 2025
Tuinuke Pamoja – Midahalo ya Kijamii Kuelekea Usawa wa Kijinsia
Na John Walter -Dodoma
Katika jitihada za kujenga jamii yenye usawa na haki kwa wote, mradi wa Tuinuke Pamoja unaotekelezwa na TGNP kwa kushirikiana na Aga Khan Foundation na kufadhiliwa na Ubalozi wa Ireland, umeendelea kuleta mwamko na majadiliano ya kina kupitia midahalo ya kijamii inayofanyika katika kata za Kidoka (Chemba), Keikei na Suruke (Kondoa).
Midahalo hii inalenga kuchambua kwa kina vikwazo vinavyozuia upatikanaji wa usawa wa kijinsia katika jamii na kutafuta suluhu endelevu kwa changamoto zinazojitokeza. Kwa kuzingatia umuhimu wa ushirikishwaji, midahalo inawahusisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa kijamii na wa dini, wazee wa mila, wazee maarufu, vikundi vya kijamii pamoja na watu wenye ulemavu.
Katika midahalo hiyo, washiriki wamekuwa wakieleza uzoefu wao kuhusu masuala ya kijinsia, mila na desturi zinazokwamisha maendeleo ya wanawake na wasichana, pamoja na mapendekezo ya jinsi jamii inaweza kuondokana na mifumo kandamizi. Kupitia mchakato huu shirikishi, jamii inahimizwa kufikiria upya mitazamo na mienendo inayozuia maendeleo jumuishi.
Mradi huu umeweka mkazo mkubwa katika kushirikisha sauti za watu walioko pembezoni mwa maendeleo, kwa kutambua kuwa hakuna usawa wa kijinsia unaoweza kufikiwa bila ushiriki wa makundi yote ya jamii.
Kwa pamoja, tunaamini kuwa "Tukiinuka pamoja, tunaweza kujenga jamii yenye usawa kwa wote."
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Mara nyingi wanawake wamekuwa watu wa kukaa kimya bila kusema wanataka nini ili kuridhishwa katika mapenzi na mbaya zaidi katika swala zima ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...




















