Wednesday, April 28, 2021
Giggs Ashitakiwa Kuwanyanyasa Wanawake
Serikali Yasitisha Matumizi ya Vitamin C Kutibu COVID-19
Kirusi Kipya cha Covid 19 ni Hatari Zaidi
Rosa Ree Akiri Kulizwa na Mapenzi
JAMAA AKUBALI KUMUOA ALIYEKUWA KAHABA NA KUZAA WATOTO 10 WA BABA TOFAUTI
Tuesday, April 27, 2021
Hali ya Mzee King Kikii Bado ni Tete “Nisaidieni”
JSC yampendekeza Martha Koome kuwa Jaji mkuu nchini Kenya
Koome ana uzoefu wa miaka 33 katika tasnia ya sheriana pia amewahi kuhudumu kamamtetezi wa haki za binadamu
Tume ya huduma kwa idara ya mahakama JSC imempendekeza jaji Martha Koome kuwa Jaji mkuu ajaye nchini Kenya ili kuichukua nafasi ya David Maraga aliyestaafu .
Kaimu mwenyekiti wa tume hiyo Olive Mugenda ametangaza kwamba uamuzi huo umeafikiwa na makamishna wote wa tume hiyo .Koome ana uzoefu wa miaka 33 katika tasnia ya sheria na pia amewahi kuhudumu kama mtetezi wa haki za binadamu . Iwapo rais Uhuru Kenyatta ataidhinisha uteuzi huo Koome atakuwa mwanamke wa kwanza kuhudumu kama Jaji mkuu nchini Kenya .
Source
Makampuni yasiyolipa waajiri kutangazwa hadharani
Na Maridhia Ngemela, MWANZA
Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, sera na Ajira, Patrobas Katambi.
,amewataka waajiri kuwathamini wafanyakazi kwani wao ndo hufanya kazi na kuinua uchumi wa taasisi husika hivyo ni vyema kuona thamani ya mwajiri na kumpatia sitahiku zake kwa wakati.
Ameongeza kuwa,wananchi kutambua,walioshikilia uchumi wa nchi ni wafanyabiashara wa kati kushuka chini,ndio maana serikali imeamua kuwawezesha,hivyo vijana,kina mama na baba wafanye kazi na sio kusubiri ajira ambazo upatikanaji wake umekuwa ni watabu.
Katambi alisema hayo jijini Mwanza alipokuwa akizungumza na waajiri ,chama cha wafanyakazi pamoja wakala wa usalama afya na mahali pa kazi ( Osha) katika maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya mahala pa kazi Duniani ambayo yalianza Aprili 26 mwaka huu hadi Aprili 28/2021 ambayo ndio itakuwa siku ya kilele,
"Waajiri wapo wanaowanyima haki wafanyakazi kujiunga na vyama vya wafanyakazi,natoa rai andapo wakibainika sisi tutawashughulikia,hivyo wale wote walioyo na madai walioumizwa na wanasumbuliwa na waajiri kupata haki yake wafike wizarani tutatatua madhira hayo,"alisema Katambi.
Katika maazimisho hayo zaidi ya wajasiliamali 600 kutoka mikoa ya kanda ya ziwa walipatiwa mafunzo ya usalama,Afya mahala pakazi kwa kipindi cha wiki mbili,ambayo yamegharimiwa na serikali maana wananchi ili afanye kazi anategemea afya na usalama ikiwa ni kuleta mafanikio ndani ya familia na Taifa kwa ujumla
Naye mkurugenzi mtendaji wa OSHA Khadija Mwenda,alisema, adha kubwa wanayokutana nayo katika usimamizi wa sheria ni uelewa mdogo wa kukabiliana na athari kazini kumepelekea matatizo,hivyo wananchi watambue mtaji wao ni usalama na afya,hivyo akipata madhara hawezi kujikomboa kiuchumi kutokana na maumivu au kilema alichokipata kutokana na mazingira ya kazi
Aidha mwenda alisema bado kunachangamoto katika mfumo ya kuwalinda wafanyakazi mpaka sasa ni asilia 40 tu ndio kubwa wako salama mahala la kazi.
Kwa upande wake wakili mwandamizi chama cha waajiri Tanzania Mercy Sevya amesema waajiri wawaelimishe kuhusiana na namna ya kuishi salama na kutoa mfumo samala kwaajili ya wafanyakazi mahala pa kazi .
AWESO ATOA SIKU 10 MRADI WA MAJI MWAKITOLYO SHINYANGA UKAMILIKE
![]() |
Waziri wa Maji Jumaa Aweso (mwenye shati la bluu katikati) akiwa kwenye ziara ya kukagua mradi wa Maji Mwakitolyo wilayani Shinyanga, wa tatu kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko. |
Waziri wa Maji Jumaa Aweso ametembelea ujenzi wa mradi wa maji Mwakitolyo uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga huku akitoa siku 10 mradi huo uwe umekamilika na kutoa huduma ya maji kwa wananchi.
Amesema kati ya miradi ya maji 177 ambayo ni kero hapa nchini, mmoja wapo ni mradi huo wa Mwakitolyo hivyo kuagiza hadi ifikapo Mei 5 mwaka huu ndani ya siku 10 zijazo, uwe tayari umeshakamilika.
"Mradi huu wa maji Mwakitolyo nina historia nao, ni kati ya miradi ya maji kichefuchefu hapa chini, hivyo naagiza hadi ifikapo Mei 5 uwe tayari umeshakamilika"
"Nakumbuka nilikuja hapa miaka ya nyuma mradi hiu ulikuwa ni changamoto nikaupa jina kichefu chefu kwa sababu haiwezekani zitokea fedha Bilioni 1.4 lakini mwananchi hana maji "Alisema
Waziri Aweso alisema mradi huo ni miongoni mwa 177 ambayo waliianisha ambayo ilikuwa inachafua wizara na maelekezo yalikuwa ni kuhakikisha miradi kichefu chefu yote inakwamuliwa na kati ya miradi 177 miradi 85 wameikamilisha ikiwemo huo wa Mwakitolyo .
Alisema hivi sasa hapo hakuna kisingizio kwa sababu fedha zimekwisha kutolea milioni 400 na mabomba yameshajengwa hivyo ndani ya Mei 10 mwaka huu wananchi wanakwenda kupata huduma ya maji.
"Hapa visingizio hakuna tena tutakwenda kugombana kwa hali ninavyoiona mambo ni mzuri kubwa ninaloliona pamoja na wananchi wa mwakitolyo kupata maji lakini na mwakitolyo maeneo ya jirani inakuwa kwa kasi sana kwa hiyo tutafute eneo la mlima tutengeneze tenki la lita laki tano"Alisema
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira katika mji wa Kahama na Shinyanga (Kahama Shinyanga Water Supply and Sanitation Authority(KASHWASA) Mhandisi Joshua Mgeyekwa, ambao ndiyo watekelezaji wa mradi kwa kushirikiana na (RUWASA),alimhakikishia Waziri Aweso kuwa utakamilika ndani ya siku hizo 10.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mara nyingi wanawake wamekuwa watu wa kukaa kimya bila kusema wanataka nini ili kuridhishwa katika mapenzi na mbaya zaidi katika swala zima ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...








