Wednesday, April 15, 2026
CRDB YAWAPA DILI NONO WATEJA: WASHINDI KUSAFIRI MAREKANI KUSHUHUDIA KOMBE LA DUNIA 2026
Tuesday, April 14, 2026
WACHIMBAJI MADINI MWABOMBA WASISITIZA UMUHIMU WA AMANI NA UTULIVU
Wachimbaji madini katika Mgodi wa Mwabomba, Kata ya Idahina, Jimbo la Ushetu, wameeleza kuwa amani na utulivu ni nguzo muhimu katika shughuli za uchimbaji, wakisema bila hali hiyo kazi zao haziwezi kufanyika kwa ufanisi wala kuleta tija kwao na taifa kwa ujumla.
Baadhi ya wachimbaji hao, akiwemo Juma Ngosha na Mabula Mayala, wamesema mazingira ya amani yamekuwa yakichochea ukuaji wa shughuli za uchimbaji, kuongeza uzalishaji na kuwavutia wawekezaji, huku wakibainisha kuwa migogoro au hali ya sintofahamu inaweza kuhatarisha usalama wao pamoja na uchumi wa eneo hilo.
Aidha, wachimbaji hao wameiomba serikali kuwapatia Soko la Dhahabu katika eneo la Mwabomba ili kuwawezesha kuuza madini yao kwa urahisi na kwa bei stahiki, badala ya kulazimika kusafiri umbali mrefu kufuata masoko yaliyopo.
Wamesema uwepo wa soko hilo utasaidia kuongeza mapato yao na kudhibiti biashara holela ya madini.
Kwa upande wake, Serikali ya Halmashauri ya Ushetu imesema ipo katika maandalizi ya kuweka utaratibu wa kuanzisha Soko la Dhahabu Mwabomba, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha sekta ya madini na kuongeza mapato ya halmashauri pamoja na wananchi.
Naye Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Emmanuel Cherehani, ameahidi kulifanyia kazi suala hilo, akieleza kuwa atashirikiana na mamlaka husika kuhakikisha wachimbaji wanapata soko litakalowarahisishia shughuli zao na kuchochea maendeleo ya eneo hilo.
ANTHONY GODFREY MARIKI : PROGRAMU YA BARRICK YA KUWEKEZA KATIKA KIZAZI KIJACHO CHA WATAALAMU WA SEKTA YA MADINI INA MANUFAA MAKUBWA KWA TAIFA
****
“Nikiwa ni miongoni mwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Johanesburg nchini Afrika ya Kusini nikisomea fani ya uhandisi wa madini kwa ufadhili wa kampuni ya Barrick Tanzania najivunia kuwa katika programu hii ya kuwapatia mafunzo wataalamu wa sekta ya madini wa siku zijazo na ninaamini ina manufaa makubwa kwa Tanzania ambayo ni nchi yenye hazina kubwa ya madini ya aina mbalimbali” anasema Antony Godfrey Mariki.
Godfrey Mariki ni miongoni mwa wanafunzi watano wa mwaka wa kwanza kutoka shule ya Madini na Sayansi ya Miamba (SoMG) katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam walioshinda ufadhili (Scholarship) ya kampuni ya Barrick yenye ubia na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals ambaye kwa sasa anasoma kozi ya uhandisi wa madini nchini Afrika ya Kusini.
Katika mahojiano yaliyofanyika karibuni kutokea nchini Afrika ya Kusini, Mariki amesema anayo furaha kuona yeye na wenzake wanaendelea vizuri katika masomo yao wakiwa wanapata msaada na ufuatiliaji wa karibu kutoka kwa mfadhili yaani kampuni ya Barrick na Chuo Kikuu cha Dar es salaam ambapo walikuwa wanasoma hapo awali.
”Ufadhili huu tuliopata naamini sio wa kifedha tu bali ni fursa ya kipekee ya kujiendeleza kitaaluma kwa kupata elimu bora kutoka chuo bora barani Afrika ikizingatiwa kuwa Afrika ya Kusini imeendelea zaidi katika sekta ya madini zaidi ya hapo katika vipindi vya likizo Barrick imetupatia fursa ya kupata mafunzo ya vitendo kwenye migodi yake ili tuweze kupata maarifa zaidi”,amesema Mariki.
Kuhusiana na progamu hii Mariki anasema kuwa Barrick imeonyesha maono yake kwa kuwekeza kwenye elimu inaolenga kuboresha sekta ya madini nchini Tazania “Kupitia program hii ni dhahiri kwamba Barrick inaanda waaalamu wazawa kutoka Tanzania watakaoendeleza na usimamia sekta ya madini katika siku za mbele ili kuhakikisha inatoa mchango mkubwa kwa ukuaji wa uchumi wa nchi sambamba na kuwanufaisha Watanzania”,amesema.
Mariki ameongeza kuwa anafurahi kuona Barrick mbali na kutoa ufadhili huu pia imekuwa na programu mbalimbali za mafunzo zinazolenga kuwajengea uwezo wataalamu wa sekta ya madini ikiwemo kuendesha semina za wanafunzi wanaosoma fani ya madini na utafii wa madini kwa kutumia wataalamu wa kampuni ambapo pia imekuwa ikitoa fursa kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kupata mafunzo ya vitendo katika migodi yake ya North Mara na Bulyanhulu.
Akielezea historia yake fupi ya elimu amesema elimu ya msingi alisoma katika Shule ya Royal iliyopo mjini Moshi na alipomaliza alichaguliwa kujiunga na Seminari ya St,James nayo ipo mkoani Kilimanjaro baadaye masomo ya juu ya sekondari katika shule ya Kisimiri ambayo imemjenga zaidi katika safari ya kutimiza ndoto yake akaweza kupata vigezo vya kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kusomea kozi aliyoipenda ya uhandisi wa Madini.
Mariki anaamini kuwa mafanikio yoyote yanapatikana kwa kuwa na bidii katika jambo lolote ambalo mtu anafanya na kutoa wito kwa vijana wenzake nchini kuchangamkia fursa zinazojitokeza kuanzia kwenye masomo,kazi,biashara na shughuli nyinginezo zote."Mafanikio yoyote maishani yanahitaji kufanya kazi kwa bidii",amesisitiza.
Anasema wakati serikali ya Tanzania inakwenda kasi katika kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya madini,kunahitajiwa uwekezaji wenye mipango mikubwa utakaowezesha miradi mbalimbali ya kimkakati inayoendelea kuanzishwa kuwa endelevu na sio tu kuwekeza kwenye fedha na teknolojia bali kuwekeza pia katika kupata wataalamu wa kuendesha miradi kwa kipindi cha sasa na miaka ya mbele.
Ameendelea kueleza kuwa kuwa bila kufanya uwekezaji wenye mtazamo wa kujenga biashara endelevu kwa miaka mingi, kuna hatari ya biashara nyingi hususani katika sekta nyeti kama za madini,usafirishaji na mafuta kuendelea kutegemea wataalamu wa kigeni na watanzania kuachwa nyuma na kubaki kama watazamaji.
Anashauri kuwa kuna haja ya kuwapatia vijana wengi wa kitanzania fursa za kusoma fani zenye wataalamu wachache katika vyuo vikuu vya ndani na nje ya nchi sambamba na kuanzishwa Progamu mbalimbali za kuwanoa vijana wa kitanzania wahitimu wa vyuo vikuu na vyuo vya ufundi kwa kuwapatia mafunzo ya vitendo kwa ajili ya kuwaanda kwendana na mabadiliko yanayotokea katika kila sekta na kushika nafasi za uongozi katika siku za usoni.
Akiongea kuhusu kupata nafasi ya Ufadhili wa Barrick kusomea taaluma ya madini nchini Afrika ya Kusini Mariki, anaeleza kuwa anajivunia kuwa miongoni mwa wanafunzi wachache waliochaguliwa kwa kuwa ushindani wa kuipata nafasi ulikuwa mkubwa sambamba na mchujo mkali uliofanywa na wataalamu mbalimbali ili kuhakikisha na kujiridhisha kuwa wanachukua watu wenye uwezo, makini na waliopo tayari kujifunza."Nina uhakika tutafanya vizuri na kupata kile kilicho bora na kukirudisha kwa taifa katika kutumikia watanzania wote kwa manufaa ya nchi ",amesisitiza.
Anasema moja ya ndoto kubwa aliyokuwa nayo katika maisha yake ni kufanya kazi katika kampuni kubwa na zenye mifumo mizuri ya kazi, jambo ambalo linaelekea kutimia kutokana na kampuni ya Barrick kutangaza pia fursa kuwapatia ajira pindi watakapomaliza elimu sambamba na kuwapatia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kufanya kazi kwa vitendo wakati wote watakapokuwa masomoni.
Kuhusu mambo yanayomvutia kutamani kufanya kazi katika kampuni ya Barrick amesema ni mengi mbali na kupata maslahi mazuri na utaalamu wa viwango vya kimataifa pia anavutiwa na jinsi inavyotekeleza mkakati wake endelevu wenye mtazamo wa kujenga jamii endelevu kwendana na utekelezaji wa malengo endelevu ya milenia ya umoja wa mataifa (MDGs).
"Inafurahisha kuona kampuni inayapa kipaumbele masuala ya msingi katika kujenga biashara endelevu kama vile utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji,usalama wa wafanyakazi wake ,kushirikiana na jamii zilizopo katika maeneo inakofanyia biashara zake kama ambavyo inafanya kazi na wazabuni wa ndani kuhakikisha inafanya manunuzi ya ndani ya nchini kwa asilimia kubwa ,kuendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa wazabuni ili nao biashara zao zikuwe na kuwa endelevu bila kusahau kufanikisha miradi mbalimbali ya kusaidia jamii hususani katika sekta za elimu, ,afya, ,maji safi na salama na uboreshaji wa miundombinu ya barabara", amesema Samson.
Mariki, anaeleza kuwa anaamini kuwa hadi kufikia kuhitimu shahada yake ya kwanza nchini Afrika ya Kusini, atakuwa amejifunza mambo mengi yatakayomsaidia katika safari yake ndefu ya kuwa mtaalamu wa madini sambamba na kuwa mbunifu na kutoa mawazo ya kitaalamu yanayowezesha kukabili changamoto na kuwezesha sekta ya madini nchini Tanzania kusonga mbele kwa mafanikio makubwa.
Amemalizia kwa kutoa ushauri kwa wawekezaji wengine wanaotoka nje na ndani ya nchi kuiga mfano wa Barrick kwa kuwa na mtazamo wa kujenga biashara endelevu sambamba na kuwa na programu za kuandaa wataalamu wazawa kwa kuwawezesha kupata elimu na utaalamu kama ambavyo imedhamini wanafunzi watano kusomea utaalamu wa fani ya madini nje ya nchi.
"Programu kama hii ni muhimu kwa kuwanoa vijana wasomi kupata ujuzi wa viwango vya kimataifa ,natamani kuona pia idadi ya vijana wanaochukuliwa katika Programu hii kuongezwa zaidi ya sasa ili inufaishe vijana wengi wa kitanzania", amesisitiza.
Picha : CHEREHANI AFANYA MKUTANO MKUBWA WA SHUKRANI USHETU, DARAJA LA MWABOMBA 99% ...MABALA ASEMA 'NI MBUNGE WA VITENDO!
@malundeblog Mbunge wa Jimbo la Ushetu Mhe. Emmanuel Cherehani amefanya mkutano mkubwa wa kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa Mbunge. Akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mabala Mlolwa, Mbunge Cherehani amesherehekea Siku ya Kuzaliwa na Wananchi wa Kijiji cha Mwabomba kata ya Idahina. Hali kadhalika amekagua daraja la Mwabomba ambalo limekamilika kwa asilimia 99 pamoja na kukabidhi fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Mwabomba! Tazama hivi Vibe!!
♬ original sound - Malunde
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...












































































