Sunday, March 16, 2025
Mzee Atapeliwa Akitaka Utajiri Kwa Mganga, Aachwa Makaburini Akiwa Uchi
Kamati yaridhishwa na Ujenzi wa Jengo la Jeshi la Zimamoto Manyara
Na John Walter -Babati
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU) imefanya ziara mkoani Manyara kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo inayosimamiwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Katika ziara hiyo, kamati ilitembelea na kukagua ujenzi wa jengo la ofisi ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani humo, ambalo linaendelea kujengwa katika Kata ya Maisaka, eneo la Katani.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, ameieleza kamati kuwa pato la mkoa huo, ambao unajikita katika sekta za kilimo, ufugaji na utalii, limeendelea kuimarika.
Pia amebainisha kuwa hali ya ulinzi na usalama mkoani humo imeendelea kuimarika, huku changamoto kubwa ikiwa ni msongamano wa mahabusu kwenye magereza.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Paul Mbogo, amesema kamati imepokea changamoto zilizowasilishwa na kwamba zitafanyiwa kazi katika bajeti ijayo ili kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kuleta manufaa kwa wananchi. 
Jengo la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Manyara litakuwa na sakafu mbili na litajumuisha ofisi saba, zikiwemo ofisi za Kamanda wa Mkoa, Kamanda wa Wilaya, Mhasibu na Masijala.
Pia, litakuwa na magari matatu yenye mitambo ya kisasa ya kuzima moto ili kuhakikisha huduma za uokoaji zinaboreshwa katika mkoa huo.
Kwa mujibu wa taarifa, gharama za ujenzi wa jengo hilo hadi kukamilika kwake ni shilingi milioni 600.6, na hadi sasa ujenzi wake umefikia asilimia 48.2.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo, amepongeza hatua ya ujenzi ilipofikia na kusisitiza kuwa kukamilika kwake kutarahisisha shughuli za uokoaji wakati wa majanga, hivyo kuokoa maisha na mali za wananchi.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, John Masunga (CDF), amesema jengo hilo litakuwa na mifumo ya kisasa ya TEHAMA, na linatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Juni 2025.
Aidha, Masunga alibainisha kuwa kituo hicho ni sehemu ya miradi saba ya ujenzi wa vituo vikubwa vya zimamoto vinavyojengwa katika mikoa ambayo awali haikuwa na vituo vikubwa vya huduma hiyo.
Ameeleza kuwa lengo ni kusogeza huduma kwa wananchi na kuhakikisha kila mkoa unakuwa na kituo cha kisasa cha zimamoto na uokoaji.
Jeshi hilo kwa sasa lipo kwenye wilaya 25 na linaendelea na mpango wa kupanua huduma ili kuzifikia wilaya zote nchini.
Mpango huo unakwenda sambamba na ununuzi wa vifaa vya kisasa vya zimamoto na uokoaji ili kuboresha utendaji kazi wa jeshi hilo.
Kamati hiyo imeishukuru Serikali kwa kutenga fedha za umaliziaji wa vituo hivyo na imewataka makamanda wa mikoa kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.
Saturday, March 15, 2025
Kijiji cha Sangaiwe Chaongoza Kitaifa kwa Ukusanyaji wa Mapato ya Utalii
Na John Walter -Babati
Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Kaganda, amepongeza juhudi za Kijiji cha Sangaiwe katika uhifadhi wa mazingira, hatua iliyowafanya kuwa vinara wa kitaifa kwa ukusanyaji wa mapato yatokanayo na utalii.
Kaganda amesema kijiji hicho ni mfano wa kuigwa katika Mkoa wa Manyara na Tanzania kwa ujumla kwa mafanikio yake makubwa ya maendeleo.
Kijiji cha Sangaiwe, kilichopo katika Kata ya Mwada, kimepata mafanikio makubwa kutokana na uhifadhi wa wanyamapori.
Kupitia mapato ya utalii, kijiji kimefanikiwa kuboresha miundombinu na kuinua hali ya maisha ya wakazi wake.
Kwa kutumia mapato hayo Kijiji kimejenga ofisi ya kisasa kwa shughuli za utawala, hatua iliyorahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi, Kila kitongoji sasa kina shule ya msingi, huku shule hizo zikiboreshwa kwa madarasa mazuri na walimu wanaolipwa vizuri kwa juhudi za kijiji.
Matokeo mazuri yameonekana kwenye sekta ya elimu, ambapo shule za msingi za kijiji zilishika nafasi ya kwanza na ya nne katika mtihani wa darasa la saba na la nne kwa ngazi ya mkoa mwaka 2024.
Kijiji kinapokea wageni 70-80 kwa siku, huku majirani zao wa Tarangire wakipokea zaidi ya 1,000 kwa siku.
Zahanati ya kisasa imejengwa kwa zaidi ya Shilingi Milioni 200, ikiwa na vifaa tiba na dawa, hatua iliyosifiwa na Mkuu wa Wilaya, Emmanuela Kaganda, kama hatua muhimu kwa afya za wananchi.
Kwa miaka mingi, wakazi wa Sangaiwe walikumbwa na changamoto ya tembo kuharibu mazao yao. 
Hili liliwasukuma kugeuza tatizo hilo kuwa fursa kwa kuingia makubaliano na wawekezaji wa sekta ya malazi ya wageni.
Mwenyekiti wa Bodi ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Burunge (JUHIBU), Patricia Mosea, amesema kijiji kimeanzisha hifadhi za jamii zinazojumuisha vijiji 10 ili kunufaika na uwepo wa tembo badala ya kuwa wahanga wa uharibifu wa mazao. 
Wakazi wa Sangaiwe wameonesha uvumilivu wa hali ya juu kwani, licha ya tembo kupita kwenye makazi yao kila siku, wamejifunza kuishi nao bila bughudha huku wakiruhusu wawekezaji kujenga hoteli kwa wageni wanaotembelea kijiji na Hifadhi ya Taifa ya Tarangire.
Kwa kipindi cha miaka miwili, Shilingi Bilioni 2.4 zimeelekezwa kwenye huduma za jamii kupitia mapato ya utalii.
Hata hivyo, kuna malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu sheria mpya ya mgao wa mapato.
Awali, vijiji vilikuwa vinapata asilimia 60 ya mapato kutoka kwa wawekezaji, lakini sheria mpya inataka wapewe asilimia 20 pekee.
Diwani wa Kata ya Mwada, Michael Mombo, pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji cha Sangaiwe, Mariani Mwanso, wamesema mabadiliko haya yanawavunja moyo wananchi na wanaomba serikali iendelee na mgao wa asilimia 60 ili maendeleo ya kijiji yaendelee kwa kasi.
Ujenzi wa shule, zahanati, na ofisi ya kijiji ni ushahidi wa jinsi uhifadhi unavyoweza kuinua maisha ya jamii.
Licha ya changamoto ya tembo na mjadala wa mgao wa mapato, wananchi wa Sangaiwe wanaendelea kufanikisha maendeleo yao kwa kauli mbiu ya Kata ya Mwada "Maendeleo Kwanza, Mambo Mengine Baadaye." "Tembo kwa Maendeleo."
Huu Hapa Msimamo wa Ligi Kuu Bara Baada ya Ushindi wa Simba Leo...
Katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliofanyika alasiri ya leo kati ya Simba SC na Dodoma Jiji FC, Simba imeibuka na ushindi mkubwa wa mabao 6-0.
Friday, March 14, 2025
Nchi Kumi Ambazo ni Vigumu kwa Mwanaume Kupata Mwanamke wa Kumuoa
JKT yatoa onyo kali kwa wanaoghushi Vyeti vya Uhitimu wa Mafunzo ya JKT
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limewaonya vijana au watu wanaojihusisha na utengenezaji wa vyeti feki vya uhitimu wa mafunzo yanayotolewa na JKT ili kuweza kupata nafasi kwenye kampuni na taasisi zinazohitaji vijana waliopitia mafunzo hayo
Hayo yamebainishwa leo Marchi 13, 2025 wilayani Chamwino Mkoani Dodoma na Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT, Kanali Juma Mrai wakati akitoa taarifa ya uwepo wa vyeti vya kughushi vya vijana waliohitimu mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria na wale wa kujitolea.
Amesema JKT imeamua kutoa onyo hilo baada ya kubaini uwepo wa baadhi ya vijana wanatumia vyeti feki kwenda kuomba kazi katika maeneo mbalimbali, ikiwemo kwenye taasisi na kampuni mbalimbali kitu ambacho ni kinyume na sheria.
"JKT tuko tayari kutoa ushirikiano kwa kampuni au taasisi yoyote inayotaka kufanya uhakiki wa watu waliotumia vyeti vya JKT kama moja ya kigezo cha kupata ajira, katika taasisi na kampuni hizo,"amesema Kanali Juma Mrai.
Amesema JKT wameanza msako mkali kuwabaini wanaojihusisha na vitendo hivyo na akisisitiza kuwa watakaowabaini watachukuliwa hatua kali za kisheria kwa kuwa wanaamini kuna stationari zinazojihusisha na vitendo hivyo na kuzitaka kuacha mara moja.
Kanali Mrai amesema JKT inatoa nafasi kwa vijana kujiunga na mafunzo hayo kila mwaka kwa vijana wa kitanzania wenye sifa ili wamalizapo mafunzo ya JKT waweze kupata cheti cha kihitimu mafunzo ya JKT kihalali.
Katika hatua nyingine amewatahadhalisha wananchi kutotapeliwa kupitia jumbe mbalimbali zinazotumwa kwenye simu za mkononi za kuombwa pesa ili wapatiwe nafasi za kujiunga na jeshi hilo na kuongeza kuwa nafasi za mafunzo hayo zitatolewa kwa njia ya mtandao na vyombo vya Habari pekee.
Thursday, March 13, 2025
UVCCM KAGERA YAIPA TANO KAULI MBIU MPYA YA CCM "KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE"

Na Lydia Lugakila - Kagera
Faris ametoa pongezi hizo katika kikao cha Baraza la UVCCM Wilaya ya Kyerwa mkoani kagera katika ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo ikiwa ni ziara ya siku 16 kutoa elimu ya uraia juu ya kupiga kura kutafuta wapiga kura wapya vijana.
Amewapongeza wajumbe wa Halmashauri Kuu Taifa walioketi Machi 10 mwaka huu kwa kupitisha kauli mbiu mpya ambayo itatumika 2025 -2030 ikiwa ni kauli mbiu mpya ambayo italeta maendeleo makubwa kwa wananchi na watanzania kwa ujmla hivyo vijana wanapaswa kuiishi na kuiweka katika mioyo yao.
Kupitia vikao mikutano mkusanyiko wa kampeni ya siku 16 mkoani Kagera elimu ya uraia kwa vijana wa CCM inaendelea kutolewa kuhakikisha wanashiriki uchaguzi mkuu ambao unatarajia kufanyika mwaka huu.
"Tunatoa elimu ya uraia kwa vijana hatubagui vijana wa rika zote ambao wamefikisha umri wa kujiandikisha kuhakisha wanajiandikisha na kupiga kura mwaka huu kwa sababu utamaduni wa vijana wengi hawapigi kura wanaongelea vijiweni ,tunaamini hii kampeini italeta mabadiliko makubwa kwa vijana sambamba na kuwaasa vijana kuchukua fomu za kugombea udiwani na ubunge ili waweze kutimiza ndoto zao," amesema.
Saturday, March 8, 2025
Eddo Kumwembe 'Mechi Inahairishwa Kwa Sababu za Kibwegebwege Sana'
Source
Bodi ya Ligi Yahairisha Michezo wa Yanga na Simba....
Kamati ya Usimamizi na Uendesha ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imetangaza rasmi kuahirisha mchezo wa Ligi Kuu namba 184 kati ya Yanga SC dhidi ya Simba SC uliyopangwa kuchezwa leo saa 1:15 usiku.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...







